LEICESTER, ENGLAND
RIYAD MAHREZ (pichani chini) anajipanga kuihama Leicester
City katika siku ya mwisho ya usajili Alhamisi baada ya kuruhusiwa kuondoka
katika Timu ya Taifa ya Algeria.Timu hiyo ya Kaskazini mwa Afrika ilitoa taarifa katika
akaunti yake ya Twitter mapema Alhamisi asubuhi, wakati muda wa mwisho wa
usajili ukikaribia.
Leicester inaamini Mahrez ana thamani ya Pauni 50 milioni,
kwa sasa alikuwa akifanya mazoezi na timu ya taifa kujiandaa na mchezo wa
kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Zambia utakaofanyika Jumamosi.
Katika taarifa yake, Shirikisho la Soka
la Algeria limesema: “Mchezaji wa Leicester City, nyota wa kimataifa wa Argeria,
Riyad Mahrez, ambaye kwa sasa yuko na timu ya taifa mjini Sidi-Moussa akijiandaa
na mchezo dhidi ya Zambia kwa ajili ya kufuzu Kombe la Dunia mwaka 2018, ameruhusiwa
Kocha wa Timu ya Taifa, Lucas Alcaraz na shirikiso la soka la Algeria kwenda
Ulaya kumalizia taratibu zake za usajili wa kujiunga na klabu mpya Alhamisi.
“Alhamisi asubuhi kikosi cha timu ya Taifa
ya Algeria kitasafiri kwenda Lusaka kucheza na Zambia, mchezo utaopigwa
Jumamosi.”
Winga huyo wa Leicester alitoa mchango
mkubwa katika ubingwa wa mwaka 2015-16 – mwanzoni mwa usajili huu wa majira ya
joto alitajwa kujiunga na Roma ya Italia lakini dili hilo lilikufa.
Klabu hiyo inayocheza Ligi ya Serie A ilishuhudia
ofa zake tatu za kutaka kumtwaa zikikataliwa na Leicester.
Wakati huohuo, Gazeti la Michezo la
Hispania AS limeandika Barcelona imemfahamisha Mahrez inamhitaji baada ya
kukwama kumtwaa Philippe Coutinho kutoka Liverpool.
Liverpool imekataa kumuuza Mbrazili huyo, ambaye kwa sasa anajianda na mchezo wa Alhamisi wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Ecuador, kwa kukataa ofa tatu – ikiwemo kubwa zaidi ya Pauni 114 milioni.
Liverpool imekataa kumuuza Mbrazili huyo, ambaye kwa sasa anajianda na mchezo wa Alhamisi wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Ecuador, kwa kukataa ofa tatu – ikiwemo kubwa zaidi ya Pauni 114 milioni.
Gazeti la AS limeripoti pia Arsenal inaweza
kumpoteza Alexis Sanchez kwa Manchester City siku ya mwisho ya usajili.
City inaweza kurudi kwa Gunners na ofay
a Pauni 70 milioni kwa ajili ya Mchile huyo baada ya ofa yao ya pauni 50
milioni kukataliwa na klabu hiyo ya Kaskazini mwa London.
Post a Comment