LIVERPOOL, ENGLAND
ALEX OXLADE-CHAMBERLAIN
amepigwa picha akiwa na jezi ya Liverpool kwa mara ya kwanza tangu
alipokamilisha usajili wa Pauni 35 milioni kutoka Arsenal.
Nyota huyo mwenye
umri wa mika 24-alifanyiwa vipimo vya afya na kukubali dili la miaka mitano
lenye thamani ya Pauni 120,000 kwa wiki ili kujiunga na vijana wanaongozwa na
Kocha Jurgen Klopps Jumatano.
Kisha Liverpool
ikathibitisha kuwasili kwa staa huyo kutoka London Kaskazini kupitia akaunti ya
Twitter, ikituma ujumbe mwepesi wa kumkaribisha sambamba na picha ya kikosi.
Akiwafahamisha mashabiki wa Liverpool kwa mara ya kwanza baada ya kuhama, Oxlade-Chamberlain alinukuliwa na Mtandao wa Liverpool: “Kwa sasa niko nje ya kambi ya England, nipo St George's Park.
...akiwa na jezi ya LiverpoolAkiwafahamisha mashabiki wa Liverpool kwa mara ya kwanza baada ya kuhama, Oxlade-Chamberlain alinukuliwa na Mtandao wa Liverpool: “Kwa sasa niko nje ya kambi ya England, nipo St George's Park.
...akifanyiwa vipimo vya afya
“Kwanza, nina furaha
ya kujiunga na Liverpool na namshukuru kila mmoja hapa katika Chama cha Soka (FA)
kufanikisha hili, kutumia vifaa. Ni msaada mkubwa sana.
“Sitasema mengi leo; niko
hapa na timu ya taifa na tutacheza michezo miwili mikubwa, kwa hiyo ninataka
kuweka akili yangu kwenye michezo hiyo. Lakini siwezi kusubiri kufika Melwood na
mtanisikia kupitia Liverpool TV.”
Post a Comment