LONDON, ENGLAND
DIEGO COSTA yuko
umbali wa maili 5,000 kutoka Stamford Bridge akiwa mbali zaidi kuunga na Kocha wa Chelsea, Antonio
Conte.
Lakini Ijumaa straika
huyo alitinga jezi ya Chelsea alipoenda kufanya mazoezi yake binafsi.
Costa kwa sasa
anafanya mazoezi ya peke yake akiwa katika mji wa asili yake wa Lagarto baada
ya kukataa kurudi England kufanya mazoezi na Chelsea.
Straika huyo mwenye umri wa miaka 28-anafanya
juu chini kuwa fiti huku akiwa na matarajio ya kurudi katika timu yake ya
zamani ya Atletico Madrid katika dirisha la usajili la Januari baada ya timu
hiyo inayoshiriki Ligi ya La Liga kufungiwa kufanya usajili.
Costa alionekana akifanya
mazoezi akiwa amevaa bukta ya Chelsea katika video aliyoituma katika Mtandoa
wake wa Instagram.
Video hiyo fupi
inamuonyesha mfungaji huyo bora wa Chelsea wa msimu uliopita kwa kufunga mabao
20, akifanya mazoezi ya kukimbia katika gym.
Pamoja na kumtaka
kurudi, tayari mabingwa hao wa Ligi Kuu wameshaziba nafasi yake kwa kumnasa,
Alvaro Morata kwa Pauni 70.6 milioni kutoka Real Madrid.
Morata yuko mbioni
kuanza katika kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza wakati timu hiyo itakapoenda
uwanjani Wembley kupambana na wapinzani wao wa Mji wa London, Tottenham
Jumapili.
Costa ameenda kwenye mji wa asili yake Brazil baada ya kufukuzwa klabuni Chelsea kwa Ujumbe Mfupi wa Maneno (SMS) na Kocha Antionio Conte. Straika huyo amegoma wito wa Chelsea kutaka arudi London.
Post a Comment