0


LIVERPOOL, ENGLAND
TOM WERNER (pichani juu) amesisitiza katika siku muhimu ya historia ya  Liverpools kwamba Fenway Sports Group (FSG) haiko kwa ajili ya kuiza klabu hiyo.
Werner, ambaye ni Mwenyekiti wa Liverpool, alikuwa uwanjani Anfield Ijumaa sambamba na mmiliki mkuu, John W Henry na Rais wa FSG, Mike Gordon katika ufunguzi wa jukwaa lenye thamani ya Pauni115 milioni, ambalo litaongeza uwezo wa uwanja huo kubeba watu 54,000.

...jukwaa lililojengwa Anfield

Jurgen Klopp(kushoto) anategemea timu kupata faida zaidi.

“Mchezo wa Jumamosi dhidi ya Leicester City umeuzwa lakini kuuza siyo sera ya FSG,” alisema Werner.

Kumekuwapo na maneno kuhusu  kampuni ya Kichina  katika majira haya ya joto lakini Werner amesisitiza siyo yeye wala washirika wake wanaoangalia suala hilo la fedha.

 Kikosi cha Liverpool kikifanya mazoezi Anfield.
“Nimeshasema mara kwa mara, hii klabu haiuzwi,” Werner alisema. “Sijui ninaweza kusema mara ngapi jambo hilo. Tunatambua hii ni changamoto, siyo kwa ajili yetu bali kwa mashabiki wetu, na kwetu ili kushindana kwenye ngazi za juu tunatakiwa kuja na ufumbuzi.


Matajiri wa Kichina walikuwa wakiitolea macho klabu hiyo na kutaka kuinunua na kuifanya kuwa tajiri kuliko Manchester City.

Post a Comment

 
Top