0


LEICESTER, ENGLAND
CLAUDIO RANIERI (pichani juu na chini) amewaambia wachezaji wake kwamba hakuna mwenye uhakika wa namba katika kikosi hicho katika kipindi hiki cha majira ya joto ambapo Leicester imejipanga kujiimarisha.

Leicester imewaongeza wachezaji wapya sita katika kutetea taji lake na Kocha Ranieri amesisitiza kuwa hiyo inamaanisha hakutakuwa na nafasi ya kudumu hata kwa upande wa wachezaji wakubwa.
Kocha huyo wa Leicester msimu uliopita alikuwa ni nadra sana kubadilisha kikosi chake wakati akisaka taji la England, alikijenga kikosi chake kupitia wachezaji 10 wakiwamamo Jamie Vardy, Riyad Mahrez na Danny Drinkwater katika michezo 30.
Lakini sasa ana uchaguzi mpana  baada ya kuwasili kwa Islam Slimani, Ahmed Musa, Nampalys Mendy, Bartosz Kapustka, Luis Hernandez na Ron-Robert Zieler, na kikosi chake kimekuwa na changamoto.
“Bila shaka hakuna uhakika wa kudumu,”alisema Muitaliano huyo. 'Hakuna kesi kwamba kwa sababu fulani alicheza msimu uliopita ana uhakika wa kucheza msimu huu. Ninaangalia kila mazoezi, naangalia kila mechi, na kama nakimuona mtu ni bora, nabadilisha kikosi.
“Hakuna mwenye uhakika wa kuvaa jezi na kuanza katika kikosi. Kila mmoj anatakiwa kuwa katika kiwango cha juu na kama mtu atashuka nitakuwa na mtu wa kumbadilisha. Hilo ndilo muhimu. 

Slimani amejiunga na Leicester kwa Pauni 29.7.


“Mwishoni siyo kikosi cha wachezaji 11 watakaokuwa wametwaa ubingwa, ni wachezaji wote, wote ni mabingwa katika Premier League. Sikumbuki nani amecheza michezo 38 na nani amecheza mchezo mmoja. Kwangu ni kundi lote limetwaa ubingwa.”

Leicester mazoezini
Jumamosi hiii, Ranieri ataingoza Leicester uwanjani Anfield  na anamini wachezaji wake wanaweza kushinda kutokana na presha waliyonayo Liverpool ya kupata ushindi baada ya kufungua jukwaa jipya uwanjani hapo.
“Wamecheza michezo mitatu nje na huu ni wa kwanza nyumbani. Watakuwa na wasiwasi wa kuonyesha ubora wao,” alisema Ranieri. 

Ranieri
“Watakuwa na wasiwasi wa ushindi. Lakini hawakuwa na uhakika wa ushindi. wanaweza, lakini pia Leicester inaweza kushinda.” 
Mbali na mchezo dhidi ya Liverpool, Leicester utaanza kucheza Ligi ya Mabingwa kwa kusafiri kuifuata Club Brugge wiki ujayo lakini Ranieri amekiri wachezaji wake hawaaanza kuyafikiria mashindano hayo.

Post a Comment

 
Top