MANCHESTER,
ENGLAND
NI
siku ya hukumu mwanzo mwisho Manchester derby huko Old Trafford
BATO
la Old Trafford. Nakwambia mtoto hatumwi dukani, hii ni shughuli ya wakubwa tu.
Manchester United na Manchester City. Jose Mourinho na Pep Guardiola. Wa kwanza
na wa tatu kwenye msimamo. Ni bato kweli kweli.
Hii
ni bato ya Manchester derby. Itapigwa mchana kweupe pale Old Trafford. Kuna
vita kubwa ya kuitazama njani ya uwanja kwa dakika zote tisini.
Jose
Mourinho v Pep Guardiola
Makocha
hao wawili kwa muda mrefu wamekuwa wapinzani. Walianza kuonyeshana ubabe kwenye
Ligi ya Mabingwa Ulaya, kabla ya vita yao kuendelea kwenye El Clasico huko
Hispania na sasa watachuana kwenye derby ya kihistoria England, Man United na
Man City kwa mara ya kwanza baada ya kujiunga na timu hizo msimu huu.
Makocha
hao kabla ya leo, wamekutana mara 16 kwenye michuano tofauti, wakiwa na timu
tofauti. Mourinho amemvaa Guardiola akiwa na Chelsea, Inter Milan na Real
Madrid, wakati Guardiola alimvaa Mourinho akiwa na Barcelona na Bayern Munich.
Vita ya leo itakuwa ya kuonyeshana ubabe nane Mfalme wa Jiji la Manchester.
David
De Gea v Claudio Bravo
Hakuna
ubishi, Guardiola atampa mechi yake ya kwanza kipa wake mpya Claudio Bravo na
mechi hiyo ni mtihani mzito kwake kuhakikisha kwamba ilikuwa sahihi kwake
kwenda kusaini Man City na kumwondoa aliyekuwa kipa wao namba moja, Joe Hart.
David De Gea ni kipa mwenye uzoefu tayari wa Ligi Kuu England na kwa misimu
kadhaa amekuwa na mchango mkubwa sana katika kuipa matokeo mazuri Man United.
Kama eneo ambalo Mourinho hakupata shida kutafuta mtu mpya ni golini kwa sababu
ya uwepo wa De Gea, Mhispaniola aliye kwenye ubora wake.
Zlatan
Ibrahimovic v John Stones
Pep
Guardiola alitua fungu la maana kumsajili beki wa kati John Stones kutoka
Everton akitegemea kupata huduma bora kabisa kutoka kwa Mwingereza huyo.
Lakini, kipimo chake cha kwanza kigumu kutambua kama kweli anastaahili kucheza
kwenye timu kubwa kama Man City ni leo atakapomkabili straika matata, Zlatan
Ibrahimovic.
Fowadi huyo wa zamani PSG hadi sasa ameshatikiza wavu mara tatu
kwenye Ligi Kuu England, tena akiwa amefunga kwa mabeki wagumu kama Wes Morgan,
Robert Huth, Jose Fonte. Je, Stones atamuweza Ibrahimovic kwa soka lake la
kibabe? Hii ni vita tamu.
Paul
Pogba v David Silva
Vita
kali zaidi kwenye Manchester derby itakuwa kwenye sehemu ya kiungo. Mahali hapa
Old Trafford itashuhudia vita ya fundi wa mpira kutoka Hispania, David Silva
akionyesha kazi na mchezaji ghali duniani, kiungo wa Kifaransa, Paul Pogba. Pogba
atataka kuwaonyesha mashabiki wa Man United kwamba hakufanya makosa kurudi
kwenye timu hiyo, tena kwa pesa nyingi, lakini Silva naye akitaka kuonyesha
kwamba kuucheza mpira ni kitu rahisi zaidi kwake kukifanya.
Vita ya nyota hao
wawili ni kwenye kuchezesha timu zao, upande upi utakuwa na mashambulizi zaidi
na kiungo gani atakuwa anatengeneza mashambulizi hayo. Hapa ni patamu pia.
Wayne
Rooney v Kevin de Bruyne
Hii
ni bato ya Namba 10. Wayne Rooney tangu Manchester United ilipokuwa chini ya
kocha Mourinho amekuwa akitumika kwenye Namba 10, akicheza nyuma ya
mshambuliaji wa kati. Kwa mahasimu wao, Man City, tangu Guardiola alipotua
hapo, Mbelgiji Kevin De Bruyne amekuwa akitumika kwenye Namba 10. Nyota hao
wawili, wote ni mafundi wa kupiga asisti, licha ya kwamba De Bruyne ni mtamu
zaidi.
Lakini, katika mechi hiyo ya leo, Rooney atakuwa nyumbani na kitendo cha
kuwa nahodha atakuwa kwenye mstari wa mbele vitani kuhakikisha Mourinho
atashinda vita yake dhidi ya Guardiola. Licha ya kwamba ni mechi ya nne tu kwenye
Ligi Kuu, lakini inabeba pia taswira kamili ya ubingwa wa msimu huu.
Anthony
Martial v Raheem Sterling
Tangu
kuanza kwa msimu huu, Raheem Sterling amekuwa kwenye ubora wake klabuni Man
City na kumfanya kocha Guardiola kumwaanzisha kwenye kikosi chake. Akitarajia
kushambulia kupitia upande wa kushoto, Man United wao winga wao wa kushoto
atakuwa Anthony Martial. Hii ni vita inayosubiriwa kwa hamu kuona ni winga gani
kati ya hao wawili atakuwa msumbufu kwa mabeki watakaomkaba, hususani mabeki wa
pembeni.
Martial bado hayupo kwenye ubora wake sana, lakini ataingia kwenye
mechi hiyo akiwa na kumbukumbu nzuri ya kufanya kweli kwenye mechi za kimataifa
akiwa na Ufaransa, hivyo atataka kuhamishia makali ya huko uwanjani Old
Trafford.
Eric
Bailly v Nolito
Pep
Guardiola atakosa huduma ya straika asilia katika mchezo huo wa Manchester
derby na hapo anaweza kumtumia Nolito kama Namba 9 feki. Hii ni staili ambayo
Guardiola amekuwa akiitumia sana akiwa amewahi kufanya hivyo kwa Lionel Messi
alipokuwa Barcelona na Mario Gotze alipokuwa Bayern Munich, huko mchezo wa leo,
Nolito anaweza kuanzishwa kama straika.
Lakini, fowadi huyo wa zamani wa Celta
Vigo hii leo hapo Old Trafford atakumbana na Eric Bailly, beki wa kati shupavu
ambaye aliwahi kukutana naye pia kwenye La Liga, wakati alipokuwa akiipiga
Villarreal kabla ya kutua Man United. Bailly tangu kuanza kwa msimu umekuwa
kwenye ubora mzuri na jambo hilo limemfanya Mourinho asihangaike kutafuta beki
mwingine wa kati baada ya kuona kwamba kombinesheni yake na Daley Blind imekuwa
tamu.
Marcus
Rashford v Kelechi Iheanacho
Rashford
na Iheanacho ni makinda bora kabisa kwenye klabu hizo kwa sasa. Makocha wao
wanaweza kuwapa nafasi katika mechi hiyo ya Manchester derby ili waonyeshe
makali yao. Rashford si mgeni wa mechi hiyo, ameshawahi kucheza na kufunga pia.
Hivi karibuni, makinda hao wote walichezea timu zao za taifa, wakati Iheanacho
akiwalaza Tanzania kwenye kuwania kufuzu Afcon 2017 alipokuwa na Nigeria,
Rashford alipiga 'hat-trick' alipokuwa na timu ya taifa ya vijana ya England na
kumfanya kocha wa timu ya wakubwa, Sam Allardyce kusema kwamba atamrudisha
kwenye kikosi cha kwanza cha wakubwa.
Kwenye timu zao, Iheanacho ameanzishwa
mara 12 tu, wakati Rashford ameanzishwa mara 18, lakini Iheanacho ameasisti
mara tano katika dakika 1291 alizocheza kikosi Man City, wakati Rashford
ameasisti mara mbili katika dakika 1452. Iheanacho ana miaka 19, Rashford miaka
18.
Post a Comment