MANCHESTER, ENGLAND
WAYNE ROONEY ameachwa katika kikosi
cha wachezaji 20 cha Manchester United kitakachocheza Europa League dhidi ya Feyenoord
Alhamisi.Mbali na Rooney, kiungo Henrikh Mkhitaryan na straika, Jesse Lingard ambao walicheza Jumamosi dhidi ya Manchester City uwanjani Old Trafford, pia hawatasafiri kwenda Uholanzi.
Mourinho
Kikosi hicho kilitangazwa kwenye
Mtandoa wa Manchester United mapema.
Rooney
Mkhitaryan alipangwa katika mchezo
huo wa upinzani ambapo Man United ilifungwa mabao 2-1 pamoja na kwamba alikuwa
akisumbuliwa na majeraha ya paja baada
ya kumaliza mchezo wa kimataifa wa kuitumikia Armenia na Kocha wa United, Jose Mourinho alitarajiwa
kuliweka wazi hilo katika mkutanono wake na waandishi wa habari Jumatano.
Ibrahimovic
Kiungo huyo hakuwepo katika mazoezi
ya timu hiyo sambamba na kikosi cha Manchester mapema Jumatano.Mabeki ambao wamekuwa na desturi ya kuanza kwenye kikosi cha United, Antonio Valencia na Luke Shaw, pia wameachwa- huku wadau wakidai kwamba nafasi kubwa itakuwa kwa Matteo Darmian, Marcos Rojo na Tim Fosu-Mensah.
Post a Comment