MANCHESTER, ENGLAND
VITA ya maneno makali
kati ya wakala wa Yaya Toure, Dimitri Seluk na Kocha wa Manchester City, Pep
Guardiola vinaonesha hakutakuwa na muafaka kati yao.
Wakala huyo wa Toure
amekataa kumuomba radhi Guardiola na kudai kwamba Mhispania huyo alikuwa na
mchanga mdogo sana katika mafanikio ya Barcelona alipokuwa kocha.
Guardiola kushoto na Yaya Toure
Seluk ameibuka tena
mbele ya jamii, saa 24- baada ya Guardiola kumtaka raia huyo wa Ukraine kumuomba
radhi kutokana na maneno yake kuhusu Manchester City.
Picha ya Kikosi cha City bila ya Yaya.
Wakila huyo wa muda
mrefu wa Toure, mteja wake amesimamishwa chini ya Guardiola ambaye amesema
hataichezea City tena hadi Seluk atakapoomba radhi.
Hata hivyo, Seluk
ameongeza petroli kwenye moto kwa kudai kwamba kiwango cha Barca kutamba
Hispania na Ulaya kimejengwa chini ya Kocha, Frank Rijkaard na Lionel Messi– na
sio bosi huyo wa sasa wa Etihad.
“Barcelona imejengwa
na Rijkaard na baadaye (Guardiola) alikuwa na bahati kwa kuwa alikuwa na
Messi,” Seluk alisema.
“Ni Messi ambaye
ameijenga Barca, siyo Pep. Kocha Luis Enrique ameonyesha mafanikio ya Barca
hayakua chini ya Guardiola.
Kocha Guardiola alishinda
mataji matatu ya La Liga na mawili ya Ligi ya Mabingwa wakati alipiokuwa Nou
Camp, na kufuatia na mataji matatu mfululizo ya Bundesliga, lakini Seluk amehoji asili ya ushindi huo.
“Hata pale Munich. Asingeweza
kufeli. Babu yangu angeweza kushinda taji la ligi akiwa na timu hiyo,” alisema.
“Kama Pep anataka kujiaminisha
kwamba yeye ni kocha mkubwa, aende Zaragoza au Sunderland. Tutaona ni mzuri atakapoacha
kuchukua timu kubwa na akiwa hapati pauni nusu bilioni za kutumia kununua
wachezaji.”
Jumanne hii, Seluk
alikubali kuingia vitani kupambana na Guardiola kwa jinsi anavyomtendea Toure
ndani ya City tangu Mhispania huyo alipowasili Etihad.
Seluk kushoto na Toure.
Awali, raia huyo Ukraine
alilamikia mteja wake raia wa Ivory Coast kunyanyaswa kwa kuachwa katika kikosi
cha Ligi ya Mabingwa, wakati Toure akiwa amecheza mchezo mmoja tu chini ya Guardiola
– mchezo wa pili wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Steaua Bucharest katika mchezo
ambao kocha huyo wa City aliwapanga wachezaji damu changa kama Pablo
Maffeo, Tosin Adarabioyo na Angelino.
Kinachouma zaidi, mchezaji
huyo bora mara nne wa Afrika hajajumuishwa katika picha ya pamoja ya klabu, ambayo
iliachiwa kwenye mitandao Jumanne.
Picha hiyo ilipigwa
wakati Toure alipokuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kipanda uso.
Uamuzi wa kuendelea
kufanya maamuzi hayo bila ya uwepo wake, unazungumzwa ni kutokana na kuongezeka
kwa uadui kati wakala na kocha wake.
Seluk alisema: “Pep hawataki
wachezaji wanaojitambua. Anawataka wachezaji wanaomuogopa na wanaofanya kile
anachokisema.
“Kitu cha kwanza
alichokifanya alipowasili City ni kuwaondoa Yaya na Joe Hart, wachezaji wawili
wakubwa klabuni. Wote wanaheshima kubwa katika vyumba vya kubadilishia nguo
klabuni Man City na Guardiola hakulipenda hilo.”
Wakala huyo alimtaka
Guardiola kumwomba radhi kipa Joe Hart
na bosi wa zamani wa City, Manuel Pellegrini kwa kuingilia kibarua chake Etihad.
Wakati sasa kukiwa na
msuguano huo na Toure amebakisha miezi minane ya kuendelea na dili lake la
kulipwa Pauni 225,000-kwa wiki klabuni
hapo.
Licha ya mkataba wake
kumruhusu kuendelea, Yaya Toure ataondoka katika dirisha la usajili la Januari.
Hata hivyo, kiungo
huyo anataka kubaki Ligi Kuu England na baadhi ya klabu kubwa za Manchester
United, Arsenal, Liverpool na Chelsea zimeonyesha nia ya kumtwaa.
Seluk alisema :“Guardiola
ameshinda michezo michache na anajiona mfalme,” Seluk alisema.
Post a Comment