0


LONDON, ENGLAND
JOSE MOURINHO na Pep Guardiola wamepangwa kukutana tena katika Manchester derby katika raundi ya nne ya Kombe la Ligi (EFL)uwanjani Old Trafford mwezi ujao.
Makocha hao wamepangwa kukutana siku 11 baada ya Guardiola wa Manchester City kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Manchester United ya Mourinho katika mchezo wa Premier League.
Ratiba ya EFL itaikutanaisha miamba mingine ya Ligi Kuu ya Premier League, Liverpool itakapoikaribisha Tottenham Hotspur na Chelsea itapambana na wapinzani wao wa London West Ham United.

Norwich ambayo iliifunga Everton uwanjani Goodison Park itasafiri kwenda Elland Road kucheza na Leeds wakati Preston iliyoifunga timu ya Premier League ya Bournemouth, itaenda Newcastle.
Miamba mingine ya Premier Leagua, Arsenal itakuwa wenyeji wa Reading wakati Hull City itasafiri hadi Kusini Magharibi kucheza na Bristol City.
Na kutakuwa na pambano lingine la timu za Premier League kati ya Southampton na Sunderland.
Ratiba ya raundi ya nne ya EFL Oktoba 24:
West Ham United
v
Chelsea
Manchester United
v
Manchester City
Arsenal
v
Reading
Liverpool
v
Tottenham Hotspur
Bristol City
v
Hull City
Leeds United
v
Norwich City
Newcastle United
v
Preston North End
Southampton
v
Sunderland

Post a Comment

 
Top