MANCHESTER, ENGLAND
MANCHESTER UNITED imeripotiwa kuwa
tayari kumlipa mishahara yake yote kiungo wake wa Kijerumani, Bastian
Schweinsteiger – yenye jumla ya thamani ya Pauni 13.8 milioni- ili kumwachia
aondoke zake Old Trafford.Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 32-amekuwa haihitajiki katika kikosi cha Kocha Jose Mourinho na amelazimishwa kufanya mazoezi na kikosi cha wachezaji wa akiba.
Pamoja na kwamba
Mjerumani huyo amebakisha miaka miwili katika mkataba wake, Mourinho amemuweka
wazi kwamba hahitajiki United.
Habari ndani ya Old
Trafford, zinasema, Schweinsteiger alitaka kulipwa mabaki ya mshahara wake kwa
jumla kama Old Trafford inataka aondoke.
Akiwa amebakisha
miezi18 na anapokea Pauni150,000- kwa wiki kwa mujibu wa mkataba wake, inaweza
kuigharimu United kama Pauni 13.8 milioni kumlazimisha mchezaji huyo kuondoka lakini
klabu inakaribia kufanya makubaliano na wawakilishi wa mchezaji huyo.
Mchezaji huyo alibaki
Manchester katika kipindi cha dirisha la usajili la majira ya joto kwa sababu
ya mshahara wake mkubwa na timu kadhaa kushindwa kumsajili.
Lakini kama malipo
hayo yatakuwa yameafikiwa kati ya Schweinsteiger
na United, mchezaji huyo wa zamani wa Bayern Munich ataweza kuwa huru kucheza
katika miaka yake ya mwisho katika klabu mpya- kinyume na anavyoteseka United
kwa kutupwa kwa wachezaji wa akiba.
Inafahamika kwamba anaweza kufungua
milango ya kwenda kucheza Ligi ya Marekani Major League kufuatia kauli yake aliyoitoa
Agosti akithibitisha kwamba United itakuwa klabu yake ya mwisho barani Ulaya.Pamoja na kufedheheshwa na kutengwa na Mourinho, Schweinsteiger hajafungua mdomo wake na kuiponda klabu hiyo na hata alionyesha nia yake ya kutembelea tena Old Trafford kabla ya kuondoka klabuni.
Post a Comment