LONDON, ENGLAND
ARSENE WENGER amesema hana mpango wa
kukisoma kitabu kipya cha Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kiitwacho ‘Jose
Mourinho: Up Close and Personal’, ambacho kimejumuisha maneno mengi ya dharau
dhidi yake.Kitabu hicho kimeandikwa na Mwandishi wa Habari, Rob Beasley ambaye amekuwa akifanya kazi karibu na Mourinho, akinukuu madai kwamba mwaka 2014, Mourinho alisema: “Siku moja nitamtafuta (Wenger) nje ya uwanja na kuuvunja uso wake.”
Wenger (kushoto) Mourinho (kulia)
Bifu
la Mourinho na Wenger lilirudi upya wakati Mreno huyo aliporejea Chelsea mwaka
2013, ambapo makocha hao kila mmoja alionyesha ubabe kwa mwenzake, ikiwamo
tukio la kukunjana mashati kwenye moja ya mechi zao.
Wenger
anaripotiwa kuchukizwa na Mourinho baada ya kumuuza Mhispaniola, Juan Mata
kwenda Manchester United na kumtuhumu kwamba anauzia maadui silaha kwa kuwa
yeye ameshacheza nao. Jambo hilo liliibua malumbano na Mourinho kutoa kauli ya
kumpasua Wenger.
Alipoulizwa maoni yake juu ya tishio
hilo, Wenger alicheka na kusema: "Sijakisoma kitabu hicho na bila shaka
sitakisoma. Kwa hiyo sitaweza kutoa maoni yangu.
... wakiamuliwa.
"Ninazungumza kuhusu soka na
hicho ndicho nitakachokifanya. Mimi si mharibifu, hapana. Nipo kwa ajili ya kujenga
na siwezi kutoa maoni kama hayo, kwa sababu ninaangalia zaidi mchezo dhidi ya
Chelsea na jinsi ninavyotaka tucheze."Kocha Mourinho aliwahi kumpachika Wenger jina na kumwita ‘Bingwa wa Kufeli’ miaka miwili iliyopita na mwaka 2015 walitaka kushikana mashati wakati bosi huyo wa Arsenal alipomsuka kifuani Mourinho katika mchezo ambao Gunners ilifungwa mabao 2-0 uwanjani Stamford Bridge.
Pia, Wenger aliulizwa kama anadhani uhusiano wake na Mourinho unaweza kuwa mzuri siku moja – kama ulivyokuwa upinzani wake wa zamani na Sir Alex Ferguson - alisema: "Siku zote ndivyo unavyoisha kama hivyo.
“Sina matatizo binafsi na mtu yeyote. Ninamheshimu mtu yeyote kwenye mchezo.
Kocha Wenger
Kocha Wenger atacheza dhidi ya Kocha
wa Chelsea, Antonio Conte kwa mara ya kwanza uwanjani Emirates Jumamosi, lakini
Wenger alisema anahisi upinzani mkali umepungua tangu kuondoka kwa Mourinho
klabuni Chelsea.
Post a Comment