0


LYON, UFARANSA
EMMANUEL ADEBAYOR ameponda madai kuwa aliagiza pombe aina ya whisky na alikuwa akivuta sigara alipokutana na mwakilishi wa mwakilishi wa klabu Lyon ya Ufaransa kwa ajili ya mazungumzo ya kujiunga na klabu hiyo.
Straika huyo wa kimataifa wa Togo mwenye umri wa miaka 32- ambaye kwa sasa hana klabu baada ya kuachwa na Crystal Palace katika usajili wa majira ya joto alikutana na klabu hiyo ya Ligue 1 wiki iliyopita jijini Lyon.

Adebayor aliwahi kuitumikia Real Madrid
Adebayor alisema, uhamisho huo ulishindikana kwa sababu Lyon ilikataa kumruhusu kuitumikia Togo katika Kombe la Mataifa ya Afrika litakaloanza Januari.
Lakini ripoti kutoka Ufaransa zinasema uhamisho huo umeshindikana kwa sababu mahitaji ya straika huyo aliyoyatoa katika mkutano huo.
Inadaiwa Adebayor alitaka ndege aina ya helikopta kwa ajili ya kumpeleka mazoezini, akodishiwe mpishi maalumu na nyumba ya kifahari yenye bwawa la kuogelea.
Kocha wa Lyon alikaririwa akisema: “Tuna sehemu maalumu kwa ajili ya kuishi kikosi chetu na Manu, niliandaa kukutana naye kwa ajili ya kunywa kahawa jijini Lyon.

... kwa hili naomba niombwe radhi.
“Lakini, kwa mshtuko, wakati alipowasili aliagiza whisky badala ya kahawa. Pia alikuwa na sigara ikining’inia mdomoni mwake.”
Hata hivyo, Adebayor ambaye ni mchezaji wa zamani wa Arsenal na Manchester City amekanusha madai hayo kabla ya kutaka kuombwa radhi.
Katika waraka wake wa Alhamisi, Adebayor alisema: “Kwa kawaida huwa sitii neno kwenye majadiliano ya uhamisho au tetesi za usajili lakini safari hii baadhi ya mambo yanatakiwa kuwekwa sawa.”
“Lyon ilitaka kunisajili na ikatoa ofa ya ndege kutoka Togo hadi Lyon kwa ajili ya kunisajili kabla ya mchezo wao dhidi ya Marseille.
“Mkataba ulikuwa umekubaliwa pande zote mbili na nilikuwa nisafiri kwa ajili ya kufanya vipimo   na kusaini fomu.
“Kwa bahati mbaya sikuweza kwenda kwa wakati na wakamsajili straika mwingine kijana badala yangu. Waliendelea kuniulizia kama ninaweza kwenda kuzungumza na kocha na mkurugenzi wao wa  soka kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa kutusajili wote.

...akiitumikia timu yake ya taifa ya Togo.
“Tulifanya mkutano Lyon lakini kocha akaona haitakuwa sawa kutusajili wote kutokana na maendeleo ya soka la vijana.
“Kwa madhumuni ya kuondoa mashaka nilikunywa maji tu katika mkutano huo na sikuagiza whisky au kuwa na sigara.”

Post a Comment

 
Top