MANCHESTER, ENGLAND
BABA MZAZI wa Yaya
Toure amemuomba Kocha, Pep Guardiola (pichani juu) kumpa nafasi kiungo huyo Muaivoricost kuitumikia
Manchester City msimu huu.
Toure amewekwa
pembeni uwanjani Eithad baada ya wakala wake, Dimitri Seluk kuingia katika
malumbano na Guardiola.
Kiungo huyo wa City ameitumikia
timu hiyo mara moja tu chini ya Guardiola katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa wa
marudiano dhidi ya Steaua Bucharest.
Pep akitoa maelekezo kwa Yaya.
Katika mchezo wa
kwanza City ilishinda mabao 5-0 tangu hapo Toure hajacheza tena.
Baba wa Toure, Mory amelisema:
“Nina wasiwasi kuhusu yeye. Ni tatatizo. Tunamuomba Guardiola kurudi chini.
“Yeye ndiye bosi. Ninamuomba
msamaha, amwache mtoto wangu afanye kazi yake.”
Kiungo mwenye umri wa
miaka 33- amebakisha mwaka mmoja tu katika mkatab wake klabuni hapo na mapema
wiki hii Guardiola alisema hatampanga katika kikosi chake hadi atakapoombwa
radhi na wakala Seluk kutokana na maneno yake kwenye vyombo vya habari.
Yaya.
Hata hivyo, Seluk alikataa
kuomba radhi baada ya kudai kwam ba Guardiola anamdhalilisha Toure kwa kumuacha
katika kikosi cha City kitakachoshiriki Ligi ya Mabingwa na kuendeleza vita ya
maneno.
Yaya Toure akiwa kazini.
Baba wa Toure
aliongeza: 'Yaya anaipenda klabu hiyo sana, ni mchezaji mzuri katika timu. Ana ari
ya kucheza.
“Siwezi kuzungumza
kwa niaba yake. Nadhani atabaki. Yeye ni mjanja. Atafanya uchaguzi mzuri
baaaye.”
Hata hivyo, City imeanza
msimu mpya vizuri bila ya uwepo wa Toure na iko kileleni katika Premier League ikiwa
na wastani wa pointi 15.
Post a Comment