0


MANCHESTER, ENGLAND
PAUL SCHOLES ameibuka tena na safari hii amemkosoa kiungo aliyevunja rekodi ya uhamisho wa dunia wa Manchester United, Paul Pogba.
Scholes kiungo wa zamani wa timu hiyo amesema Pogba hachezi kama mchezaji ambaye United imemnunua kwa Pauni 100 milioni.

Pogba
Baada ya kung’ara katika mchezo wa kwanza dhidi ya Southampton uwanjani Old Trafford, Pogba hajafanya vizuri katika michezo miwili, ule wa Ligi Kuu dhidi ya Manchester City ambapo United ililala mabao 2-1 na wa hivi karibuni wa kipigo cha bao1-0 dhidi ya Feyenoord katika Europa League.
“Ameonyesha jitihada ndogo sana mpaka sasa,” alisema Scholes. “Usiku huu, tena, hakuwa na katika kiwango bora. Nadhani atakuwa vizuri. Bado ni mapema sana. 
“Kuna wakati sikuwa nafahamu anacheza katika nafasi gani. Amefiti kwenye nafasi anayocheza?  Ameambiwa acheze anapotaka?

Scholes mwenye kipaza sauti.
“Anajaribu kuwapo kila sehemu  kwa wakati mmoja. Nadhani anajaribu kufanya mambo mengi akiwa na mpira. 
“Anajaribu kuwapita wachezaji watatu, wanne. Anakimbia na mpira. Anawezan kufanya kazi ikawa nyepesi zaidi.
“Huyo siyo mchezaji ambaye Manchester United iliyomnunua. Hawakumnunua Lionel Messi ambaye anapiga chenga wachezaji watano na kusimama kwenye kona muda wote.
“Wamemnunua kiungo mwenye nguvu, imara ambaye anaweza kupora mipira. Ana akili, anaweza kupeleka mipira mbele, anaweza kukimbia.”

Pogba dhidi ya Man City
Lakini Scholes hana wasiwasi na uwezo wa kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23. 
“Kama anaweza kucheza mara moja na kuachia, kupeleka mipira kwa Zlatan (Ibrahimovic) na kukimbia, hakuna atakayemuweza,” alisema. “ Ana kasi na nguvu sana.”
Pamoja na kusajili wachezaji wanne katika dirisha la majira ya joto, Scholes anaamini klabu yake hiyo ya zamani inambidi kurudi sokoni kumaliza tatizo la Pogba.
Scholes alisema Mfaransa huyo anateseka kwa sababu ya kukosekana kwa mchezaji mbunifu na mwenye nguvu katika kikosi cha United.

Modric
Kiungo huyo mchezeshaji mwenye mfano wa Andrea Pirlo- Muitaliano mwenye kipaji aliyekuwa akiendesha mambo na kuwa injini ya Juventus enzi Pogba akiwa na vigogo hao wa Turin. 
“Anahitaji kuwa sambamba na kiungo mwenye kontroo,” alisema Scholes. 
“(United) wanahitajika kwenda sokoni kwa ajili ya kumnunua mtu kama huyo. Michael (Carrick) anao uwezo huo.
“Lakini bado anahitaji kiungo huyo mwenye uwezo wa kumiliki, anayeweza kumlinda kila Paul anapokwenda na kumiliki mchezo wa soka.

Kroos
“Najua (Mourinho) ana furaha na wachezaji wanne aliowanunua lakini bado anahitaji aina hiyo ya mchezaji. Luka Modric au Toni Kroos (viungo wa Real Madrid) wanafaa. 
“Nadhani hawa wachezaji wanapatikana. Nadhani Pogba atakuwa bora zaidi akicheza na aina hiyo ya wachezaji.”

Post a Comment

 
Top