MANCHESTER, ENGLAND
JOSE MOURINHO (pichani chini) ametoa
sababu ya kufungwa kwa timu yake ya Manchester United Jumapili baada ya kuambulia
kipigo cha tatu ndani ya siku nane.
Kocha huyo wa United
amewatupia lawama wachezaji wake kwa kushindwa kujifunza kutokana na makosa ya mchezo wa Manchester
derby ambapo timu yake ilifugwa maboa 2-1.
Na akamtupia lawama
beki wake wa kushoto, Luke Shaw kwa kushindawa kutimiza majukumu yake dhidi ya Camilo
Zuniga.
“Nilijua nitakuwa na
kazi,” alisema Mourinho, ambaye hajawahi kufungwa michezo mitatu mfululizo tangu
alipokuwa kocha wa Porto mwaka 2002.
Mourinho akizungumza na Shaw.
“Lakini bao la kwanza
la Man City na bao hili la (Watford) pili yanafanana, unaweza kuona kuna
kufanana kwa ajabu.
“(Aleksandar) Kolarov
alipata mpira katika mazingira magumu katika kona na wachezaji wangu badala ya
kwenda kumkaba walimwachia nafasi. Leo katika bao la pili, (Nordin) Amrabat akiwa
upande wa kulia, beki wetu wa kushoto (Shaw) alikuwa umbali wa mita 25, badala
ya mita tano. Lakini pamoja na kuwa mita 25, unatakiwa kukimbia na kukaba. Lakini
hapana, tumesuburi.
“Hii ni suala la
ufundi lakini pia ni tabia ya akili ya mtu. Katika wiki kadhaa, kila kitu kama
hiki kitakuwa sawa. Hii ni kazi yangu.”
Shaw akiwa umbali mita 25 na Nordin Amrabat.
Mourinho pia alipatwa
na shaka na kiwango kilichooneshwa na wachezaji wake katika kipindi cha kwanza,
alikiri kwamba alitegemea kiwango bora baada kufuatia vipigo vilivyofuatana vya
Manchester City katika Ligi Kuu na Feyenoord katika Europa League Alhamisi iliyopita.
“Ilikuwa ni mwanzo wa
mchezo ambapo walipata nafasi nzuri za kufunga. Hilo linakatisha tamaa. Kulikuwa
na kutokuelewana kati ya kipa David de Gea na beki Chris Smalling- wachezaji wawili
wakubwa wenye uzoefu, kunakuwa hakuna mawasiliano.”
Mourinho pia
alimtupia lawama mwamuzi wa mchezo huo, Michael Oliver, akilalamikia kuachia
faulo aliyofanyiwa, Anthony Martial na kuifanya Watford kufunga bao la kuongoza
lililopachikwa na Etienne Capoue.
Mourinho aliong eza: “Makosa
ya mwamuzi na msaidizi wake hayako katika uwezo wangu. Siwezi kufanya chochote.
Katika kipindi cha pili tulikuwa bora, tulisawazisha na baada ya hapo kipa wa Watford
(Heurelho) Gomes aliokoa shambulizi na bahati ni jambo ambalo hatuwezi kulidhibiti.
Shaw akiwa ameachwa huku Zuniga akifunga bao la pili.
“Hatuwezi kumdhibiti
mwamuzi, hatuwezi kudhibiti bahati.”
Mourinho alikumbushia
kitendo cha mwamuzi kukataa penalti ya United dhidi ya City na bao la kuotea la
Feyernoord.
Post a Comment