LIVERPOOL, ENGLAND
JURGEN KLOPP anaumiza
kichwa na kishindwa kuamua kipa yupi ampange langoni wikiendi hii kati ya Loris
Karius na Simon Mignolet wakati timu hiyo itakapokabiliana na Hull City.
Kipa Karius alisajiliwa
kwa Pauni 4.7 milioni kutoka Mainz ya Ujerumani katika dirisha la majira ya
joto, ili kumpa changamoto Mignolet alicheza michezo ya maandalizi kabla ya kuvunjika mkono, alipangwa kuchukua namba katika Premier League ili
kumpa changamoto Mignolet kupigania namba.
Mignolet akimpongeza Karius.
Hata hivyo, baada ya
kuwekwa benchi michezo miwili ya ligi alionyesha upinzani katika mchezo wa
ushindi wa Kombe la Ligi (EFL) dhidi ya Derby.
Hata hivyo, Kocha Klopp hajajifunza
zaidi kwa kipa huyo Mjerumani, ambaye amekuwa akitawala mipaka ya nje ya eneo
lake la hatari, katika mchezo wa ushindi wa mabao 3-0 kutokana na kazi ndogo aliyoifanya katika
mchezo huo kwani aliokoa
hatari moja dhidi ya straika, Darren Bent na kucheza krosi moja tu kati ya
mbili.
Karius bado hajapata changamoto za kutosha.
Kipa Mignolet amekuwa
akiitumikia timu hiyo ndani ya miaka miatatu uwanjani Anfield lakini kiwango
chake hakikuwa cha kuridhisha, na kutoa nafasi ya kuletewa mpinzani wa kumpa
changamoto.
“Siyo suala la kutangaza kikosi lakini tunapaswa kufikiria kwa njia sahihi,”
alisema Klopp.
“Sijawahi kuwa kipa –
baba yangu alikuwa kipa kwa hiyo nina uzoefu kidogo katika nafasi hiyo- lakini
kwa kiasi fulani ni tofauti na wachezaji wa ndani ambao hakuna anayeweza
kuuliza kama anaanza na mwingine akaanza wakati mwingine.
Mignolet akiwa benchi dhidi ya Derby.
“Sina uhakika,
nitafanya uamuzi wa mwisho kwa ajili ya mchezo unaofuata lakini hamiaanishi
tutaendelea hivyo kwa miaka mitano ijayo.
“Ni uamuzi wa kiwango
cha juu kwa sababu ninafurahishwa
na wote wawili lakini hakuna ninaloweza kusema zaidi kuhusu hilo hapa.
“Kama ninavyofanya
kila siku kwa ajili ya mchezo unaofuata ni uamuzi wa kwa ajili ya mchezaji na
siyo dhidi ya mchezaji mwingine – mnapaswa kusubiri na mtaona.”
Mchezaji mwingine ambaye pia
anapaswa kusubiri na kuona kama atajumuishwa kwenye kikosi cha Jumamosi ni Daniel Sturridge, ambaye
alikosa mchezo wa ushindi dhidi ya Derby baada ya kutofanya mazoezi.
Karius akiokoa hatari mbele ya Bent.
“Daniel amefanya kitu
fulani kama jaribia la mwisho jana, kwa hiyo ana siku tatu bila ya kufanya
mazoezi lakini anatakwia kufanya mazoezi
leo,” alisema Klopp.
“ Kuna masuala kadhaa
baada ya mchezo (wa Chelsea Ijumaa). Kwa sasa tuna siku mbili nyingine hadi
Jumamosi na tutaona nani amefanya mazoezi muda wote na yuko tayari kwa mchezo.
Kocha Klopp.
“Ni kwamba (kucheza
kwa Sturridge) kutatokana na mazoezi. Adam (Lallana) na Gini (Wijnaldum) hawakucheza
(dhidi ya Derby) lakini watakuwa tayari.”
Post a Comment