0


MANCHESTER, ENGLAND
ZLATAN IBRAMOVIC  amempandisha presha kipa wa Manchester City, Claudio Bravo kabla ya mechi ya Manchester derby Jumamosi.
Straika Ibrahimovic anatarajia kuongoza safu ya ushambuliaji ya Manchester United katika mechi hiyo ya mahasimu itakayopigwa Old Trafford ambapo Jose Mourinho na Pep Guardiola watakutana uso kwa uso kwa mara ya kwanza kwenye Ligi Kuu England.

Wakati dunia nzima ikisubiri mechi hiyo, Ibrahimovic ameanza kumchokoza Bravo, ambaye inaaminika atakuwa golini kwenye mechi hiyo.
Fowadi huyo mwenye umri wa miaka 34 alituma video kwenye ukurasa wake mtandao wa kijamii akionekana akimtumia vifaa vya mazoezi kipa Bravo kwa sababu atakuwa anavihitaji kabla ya kumkabili Jumamosi.
Kisha Ibra aliandika ujumbe huu: “Karibu Manchester! Vifaa vya mazoezi hivyo hapo, najua utavihitaji sana. Tuonane Jumamosi.”

Kipa wa Man United, Bravo.
Ibrahimovic tayari ameshafunga mabao matatu katika Ligi Kuu England msimu huu na sasa anasubiri kuonyesha makali yake dhidi ya kipa Bravo kwenye mechi hiyo ya Manchester derby.

Post a Comment

 
Top