LONDON, ENGLAND
ALEXIS SANCHEZ (pichani juu) amesema ana uwezo sawa
na wachezaji wawili bora wa dunia, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wakati
akiwa katika majukumu ya kimataifa ya kuitumikia Chile.
Tangu ajiunge na Arsenal akitokea
Barcelona kwa dili la uhamisho la Pauni
31.7 milioni, fowadi huyo amefunga mabao 43 na kutoa asisti 25 katika michezo
96, ajijengea jina na kuwa nyota wa Emirates.
Sanchez alitoa kauli hiyo alipokuwa
katika mahojiano baada ya Chile kukatisha tamaa na kutoka sare bila ya
kufungana dhidi ya Bolivia.
“Nimefikia kiwango ambacho ninaweza kushindana na wachezaji wakubwa,” alisema Sanchez. “Sijisikii kumhofia mtu yeyote.”
“Nimefikia kiwango ambacho ninaweza kushindana na wachezaji wakubwa,” alisema Sanchez. “Sijisikii kumhofia mtu yeyote.”
“Najifananisha (kiwango changu) na Messi
na Ronaldo. Nina uwezo sawa kama wao.”
Mastaa Messi na Ronaldo wamekuwa wakibadilishana tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia ya Ballon D'or tangu mwaka 2008.
Mastaa Messi na Ronaldo wamekuwa wakibadilishana tuzo ya Mchezaji Bora wa Dunia ya Ballon D'or tangu mwaka 2008.
Katika Ligi ya La Liga msimu wa 2015-16,
Messi na Ronaldo walichangia mabao mara mbili zaidi ya yale ambayo Sanchez aliyafunga
katika Premier League.
Messi alifunga
au kuchangia 1.39 katika kila dakika 90 na Ronaldo alichangia 1.3, wakati
Sanchez alichangia wastani wa 0.63.
Maneno hayo ya Sanchez yanaweza
kuwashangaza baadhi ya watu baada ya raia huyo wa Chile kushindwa kuwamo katika
timu ya Wachezaji Bora wa Kulipwa (PFA) katika Premier League msimu uliopita, ingawaje
alijumuishwa mwaka mmoja nyuma.
Akiwa amebakisha miaka miwili katika
mkataba wake, mashabiki wa Arsenal wanatarajia klabu yao itaingia naye katika
majadiliano ya kuongeza mkataba mpya haraka.
Habari za ndani ya Arsenal, zinadai Sanchez
anahitaji kupewa mkataba wenye maslahi sawa kama wa Mesut Ozil, ambaye pia
mkataba wake unaisha 2018.
Post a Comment