0
MANCHESTER, ENGLAND
MINO RAIOLA amesema straika wa Manchester United, Zlatan Ibrahimovic alimtishia kumvunja miguu kama asingemruhusu Paul Pogba kutua Manchester United.
Wakala Raiola ambaye anawawakilisha wachdezaji hao wawili sambamba na Henrikh Mkhitaryan alisema hata hivyo Ibra alizungumza kwa utani.
Wakala huyo aliandaa  mikataba ya nyota wote watatu kutua United katika usajili wa majira ya jotoin – na Pogba akivunja rekodi ya dunia kwa kusajiliwa kwa Euro105 milioni.

Pogba na Ibra.
"Zlatan aliniambia, ‘ukifanya uhamisho wa Pogba sehemu nyingine nitavunja miguu yako'," alisema Raiola.
Wawili hao wamemfanya Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kuwa na uchaguzi mpana wa kupanga kikosi chake uwanjani, lakini Ibrahimovic amezoea haraka na amewafungia ‘Mashetani Wekundu’ mabao manne.
Pogba anapaswa kupambana kuweza kujenga jina Old Trafford.
Hata hivyo Mfaransa huyo ameonyesha kiwango cha thamani, baada ya kufunga bao  katika ushindi wa mabao 4-1dhidi ya mabingwa watetetezi Leicester City, Jumamosi.

Mourinho.
Kabla ya mchezo huo, Raiola, alionyesha hisia zake kwamba Kocha Mourinho hamchezeshi Pogba katika nafasi yake sahihi, ambako ni kushoto kwa washambualiji watatu.
"Pogba bado anapaswa kutafuta sehemu yake kwenye timu," Raiola alisema. "Napendekeza nafasi ya kiungo mshambuliaji wa kushoto.
"Kutokana na nguvu zake, stamina na ufundi... Pogba ataweza kumudu jukumu lake. Lakini  Mourinho anatakiwa kufanya uamuzi."


Ibrahimovic.
Nahodha Wayne Rooney akiachwa benchi dhidi ya Leicester na Pogba akachukua jukumu la kutengeneza mashambulizi, kiwango kilishoonyeshwa Jumamosi itabaki ni shauri la Mourinho kuendeleza hadi mwishoni mwa msimu.

Post a Comment

 
Top