MANCHESTER,
ENGLAND
JOSE
MOURINHO (pichani chini) ameshapata nguvu ya kuweka mambo sawa baada ya Manchester United
kuichapa Leicester City mabao 4-1 Old Trafford Jumamosi mchana na sasa amefanya
kikao cha dharura na kumpiga biti nahodha wake, Wayne Rooney.
Mourinho
alikuwa katika presha ya hali ya juu baada ya United kuchapwa mechi tatu
mfululizo, lakini baada ya kumuweka Rooney benchi katika pambano la Leicester
amepata nguvu ya kufanya naye mazungumzo ya moyoni na kumuonya jambo.
Kocha
huyo Mreno amemwambia Rooney kwamba analazimika kwanza kurudisha fomu yake
kabla ya kufungua mdomo wake kulalamikia viwango vya wachezaji wengine katika
timu hiyo akiwa kama nahodha baada ya kucheza ovyo siku za karibuni.
Inadaiwa
kuwa Rooney alitoa maneno makali wakati wa mapumziko wa pambano kati ya
Manchester United na watani zao Manchester City lililopigwa wiki mbili
zilizopita ambapo timu hiyo ilikuwa imechapwa mabao 2-0 hadi kufikia wakati wa
mapumziko.
Na
sasa imebainika kuwa Mourinho alimuita Rooney katika ofisi yake iliyopo uwanja
wa mazoezi wa United, Carrington na kumwambia kuwa amepoteza haki ya kuwalaumu
wengine mpaka yeye mwenyewe atakaporudisha kiwango chake.
Rooney
pia ameambiwa kuwa atalazimika kupigania nafasi yake baada ya wachezaji
waliopewa nafasi yake Jumamosi kuonyesha uwezo mzuri kiasi cha mashabiki na
wachambuzi wengi kuhoji kama mchezaji huyo ndiye anayeirudisha nyuma timu hiyo
pindi anapoanza mechi.
Rooney
Rooney
alipumzishwa katika pambano la kwanza la Europa la United dhidi ya Fayenoord
jijini Rotterdam hivi karibuni, lakini alipopewa nafasi katika pambano la
Watford alionyesha kiwango kibovu huku United ikichapwa mabao 3-1.
Rooney na Mourinho
Alicheza
tena katika pambano la Kombe la Ligi dhidi ya Northampton Jumanne iliyopita
lakini hakuweza kuthibitisha makali yake huku United ikishinda kwa mabao 4-1
dhidi ya vibonde hao. Na sasa nafasi yake iko hatarini Old Trafford.
Mourinho
alidai kwamba alimuacha Rooney katika pambano dhidi ya Leicester City kwa
sababu alihitaji wachezaji wenye damu inayochemka zaidi, Marcus Rashford, 18,
na Jesse Lingard, 23 kwa ajili ya kumchezesha mshambuliaji mkongwe, Zlatan
Ibrahimovich.
Mourinho, Rooney mazoezini.
Huku
Juan Mata akichezeshwa namba 10 ambayo imekuwa ikichezwa na Rooney katika siku
za karibuni, United ilirudi katika ubora wake katika pambano hilo ambalo hadi
mapumziko walikuwa wanaongoza kwa mabao hayo manne kwa mshangao wa mashabiki
wengi wa soka duniani walioamini kuwa mechi hiyo ingekuwa ngumu kwa United.
Rooney
anatazamiwa kurudi uwanjani katika pambano la Europa dhidi ya Zorya Luhansk,
lakini kuna uwezekano mkubwa asianzishwe tena na Mourinho katika pambano la
Ligi dhidi ya Stoke City ugenini Jumapili.
Post a Comment