0



LONDON, ENGLAND


EDDIE HOWE ndiye kocha anayepewa nafasi kubwa ya kuubeba msalaba wa Arsenal Wenger ndani ya Emirates.
Kocha huyo Mwingereza kwa sasa anakionoa kikosi cha Bournemouth na ndiye anayejadiliwa sana kwenye korido za Emirates kuwa  anafaa kurithi mikoba ya Mfaransa, Arsene Wenger wakati atakapong'atuka ukocha na kupandishwa nafasi za juu klabuni hapo.

Kocha Wenger akiwa na Howe.
Howe anawavutia wengi kwenye klabu hiyo ya ikiwamo wafanya maamuzi katika klabu hiyo ya Ligi Kuu England.  Howe aliisaidia Bournemouth isishuke daraja msimu uliyopita, anafuatiliwa sana na Arsenal inavutiwa kwa namna anavyofanya mambo yake uwanjani.
Mkataba wa Wenger unafika tamati mwishoni mwa msimu huu na hakuna mazungumzo ya kuongeza mwingine, licha ya kwamba Mfaransa huyo aliambiwa na mmoja wa wamiliki wa klabu hiyo, Stan Kroenke kwamba anaweza kuendelea kubaki klabu hayo, huku wakiamini Howe anaweza kuingoza timu hiyo kama Wenger ataamua kung'atuka.

Howe
Wenger ambaye analipwa Pauni 7.5 milioni kwa mwaka ameambiwa kwamba ana kibarua cha maisha yake yote klabuni hapo akitengenezewa nafasi ya kuwa mkurugenzi wa ufundi pindi kocha mpya atakapopatikana.
Wenger, amempeleka kwa mkopo kiungo Jack Wilshere kwenda Bournemouth hiyo inatokana na kupendezwa na utendaji wa Kocha Howe.

Post a Comment

 
Top