MANCHESTER,
ENGLAND
ZLATAN IBRAHIMOVIC amedai
kati ya timu zilikuwa zikimtolea macho ili atue katika Premier League ni pamoja
na Arsenal ya Arsene Wenger.
Straika huyo aliweka
wazi kuwa kulikuwa na ofa zilizowekwa juu ya meza kutoka Arsenal na Manchester
City kabla ya kufanya uamuzi wa kujiunga na 'Bwana Mipango', Jose Mourinho.
Ibrahimovic
Straika huyo mwenye
umri wa miaka 34- alijiunga na Manchester United katika majira haya ya joto
pamoja na kwamba amekuwa akiwindwa kwa muda mrefu kutua Premier League.
Ibrahimovic aliweka
wazi kwamba kucheza England sio kitu ambacho alikuwa akikihitaji sana hadi
kilipofika kipindi cha majira haya ya joto.
Mpaka sasa Ibrahimovic amefunga mabao manne katika michezo minne tangu alipowasili Old Trafford na anajipanga kuanza katika Manchester ‘derby’ dhidi ya Pep Guardiola wa Man City Jumapili mchana.
Mpaka sasa Ibrahimovic amefunga mabao manne katika michezo minne tangu alipowasili Old Trafford na anajipanga kuanza katika Manchester ‘derby’ dhidi ya Pep Guardiola wa Man City Jumapili mchana.
Kocha Wenger
Ibra anasema hakuwa
na mawazo yoyote ya kutua Arsenal na City
miaka hiyo ya nyuma.
'Nilikuwa karibu
kutua Premier League mara mbili – mara ya kwanza Arsenal na baadaye Manchester
City,” Ibrahimovic alisema.
“Lakini kamwe
haikutokea na sikuhitaji kucheza Premier League,” alisema Ibrahimovic ambaye
anajipanga kusomea ukocha ili akistaafu
aweze kukaa katika benchi la Manchester United.
Post a Comment