0


MADRID, HISPANIA
DIEGO SIMEONE (pichani) anaonekana kujipanga kuondoka Atletico Madrid mwishoni mwa msimu ujao lakini klabu za Ligi Kuu England zitashindwa kumnasa.

Inadaiwa kwamba kocha huyo Muargentina mwenye mafanikio makubwa amejipanga kutua Italia.
Baadhi ya vyombo vya habari vya Hipsania vimeripoti Alhamisi kwamba, Simeone amechukua  uamuzi wa ajabu wa kupunguza mkataba wake kwa miaka miwili na sasa atakuwa huru mwaka 2018 badala ya aliokuwa amejifunga awali hadi 2020.
Mabadiliko hayo yana nia ya kuhitimisha kile kilichomfanya kukaa katika klabu hiyo kwa miaka saba.
Kocha Simeone ndiye aliyedumu kwa muda mrefu Hispania na ameshinda mtaji matano akiwa na Atletico na ameipeleka timu hiyo katika fainali mbili za Kombe la Ulaya na ameweka alama yake kwenye historia ya klabu hiyo kama mmoja wa makocha wakubwa.

Kocha Simeone ambaye pia ni nahodha wa zamani wa klabu hiyo na mshindi mara mbili haondoki vibaya na anafahamu anaondoka mwaka 2018 itafanya kuiona klabu hiyo ikitumia uwanja wake mpya wenye uwezo wa kuingiza watazamaji 67,000 msimu ujao.

Pia, Kocha Simeone ataondoka akiwa amepitia kipindi kigumu cha miezi 18 bila ya kuruhusiwa kusajili mchezaji mpya baada ya rufaa ya klabu hiyo dhidi ya Fifa kutupiliwa mbali.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 46- nahodha wa zamani wa Argentina alisaini dili la kuionoa Atletico Madrid Machi 2015 hadi 2020 lakini alikiri baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita kwamba ataangalia mustakabali wake.
Na chanzo cha ndani ya klabu hiyo kimesema kwamba, Atletico imefanya kazi kubwa kumbakisha katika majira ya msimu wa joto.
Klabu mbili za Paris Saint Germain na Inter Milan zimekuwa zikivutiwa na huduma yake lakini hakuna kati yao walioweza kumnasa. Simeone alikwa akisita kuhamia PSG na mkatana wake mrefu  lilikuwa likimaanisha fidia kubwa iliyoiweka mbali Inter.

Mchezaji huyo wa zamani wa Ligi ya Italia ya Serie A, ameipa nafasi Italia kama sehemu yake atakayotua na Inter inaweza kumpata bure, baada ya kupunguza mkataba wake kama itaweza kusubiri hadi 2018.

Post a Comment

 
Top