LONDON,
ENGLAND
DIDIER
DROGBA (pichani chini) hawezi tena kuitambia Arsenal uwanjani, lakini anaweza kuitupia maneno
katika mitandao ya kijamii kama alivyomtupia Theo Walcott katika Mtandao wa Twitter.
Mambo
yote yalianza baada ya winga wa Arsenal, Walcott ambaye ameanza kwa mafanikio msimu
huu baada ya kufunga bao la pili na kuiangamiza Chelsea katika ushindi wa mabao
3-0.
Katika
kudhihirisha furaha yake baada ya mchezo huo, Walcott alipo-posti picha katika
Mtandao wa Twitter akishangilia na kuisindikiza na maelezo ya kufurahia bao
alilofunga.
Hata
hivyo, Drogba ambaye hakufurahishwa na kiwango cha Chelsea alimpongeza na kasha
akamjibu: “Hongera kaka @theowalcott, lakini ni rahisi kwa panya kutamba
baada ya paka kuondoka.”
Enzi
zake, Drogba aliinyanyasa Arsenal alipokuwa Stamford Bridge, akifunga mabao15 katika
michezo 16 kati ya mwaka 2004 na 2012.
Walcott akishangilia bao lake.
Kama
haitoshi alifunga tena dhidi ya Arsenal katika michezo wa maandalizi ya msimu
ilipofanya ziara Marekani, ambako alipopangwa katika kikosi cha kwanza cha
wachezaji wa Ligi ya Marekani, MLS All-Stars katika kipigo cha mabao 3-1.
Kabla
ya ushindi wa Jumamosi uwanjani Emirates, Arsenal iliifunga Chelesea mara moja
katika miaka mitano mwaka 2011- wakati, Cesc Fabregas alipokuwa nahodha wao.
Post a Comment