MADRID, HISPANIA
CRISTIANO RONALDO wa Real Madrid amefura kwa hasira baada ya kutolewa
uwanjani na
kocha wake, Zinedine Zidane katika mchezo wa sare dhidi ya Las Palmas.
Ronaldo
alishangaa huku akionyesha hasira za wazi alipotolewa katika dakika 72 katika
mchezo huo wa Jumamosi usiku– ikiwa ni mara ya kwanza ndani ya miaka saba tangu
alipoanza kucheza soka.
Kocha
Zidane alimpa mkono Ronaldo wakati akitoka uwanjani, lakini Mreno huyo
aliupokea bila ya kukutanisha macho na kocha wake. Moja kwa moja alikwenda
kukaa kwenye benchi akiwa amefura kwa hasira.
Ronaldo akikwepa kumwangalia Zidane.
Na
uamuzi huo, uliwasha moto baada ya mchezaji wa zamani wa Barcelona B, straika wa
Las Palma, Sergio Araujo kusawazisha bao na kufanya matokeo yawe 2-2.
Hata
hivyo, Zidane alitetea uamuzi wake wa kumtoa Ronaldo na kukanusha kwamba
straika huyo alichukizwa na kitendo hicho.
...akiwa uwanjani.
"Sio kama (Ronaldo) alicheza vibaya,"
alisema Zidane na kuongeza : " Tunacheza Jumanne na wakati mwingine Cristiano
anatakiwa kupumzika. Ilikuwa ni kwa ajili hiyo. Alicheza vizuri. Usiku nilimwangalia na
kufikiria mchezo wa Jumanne.
Ronaldo akitoka...
"Hasira?
Hiyo itakuwa ni tafsiri yenu. Kila siku anataka kuwa uwanjani. Huwa tunamtoa wakati
mwingine, na tumefanya hivyo leo. Haikubadilisha kitu."
Post a Comment