0
MADRID, HISPANIA
CRISTIANO RONALDO (pichani) amemshukia Xavi Hernandez baada ya kiungo huyo wa zamani wa Barcelona kudai Ronaldo ana bahati mbaya kuzaliwa katika kipindi ambacho Lionel Messi amezaliwa.
Kiungo Xavi alimsifu Mreno huyo kwamba ni mchezaji mzuri, lakini alisema ana bahati mbaya ya kuzaliwa kipindi ambacho nyota wa Argentina amezaliwa.

Ronaldo akishangilia bao
Ronaldo alisaidia timu yake kuifunga Osasuna mabao 5-2 akiwa ndio kwanza anarudi kutoka katika majeraha. 
Straika huyo aliumia  katika mchezo wa fainali ya Uero 2016 dhidi ya Ufaransa.
“Mchezaji anayetafutwa sana kwenye mtandao ni mimi,” alisema kwa hasira Ronaldo. “Wanaotaka kutokea kurasa za mbele (katika magazeti) au kutangaza vitu wanazungumzia kuhusu mimi.
“Nitajari kitu gani ambacho Xavi anasema? Anacheza wapi? Qatar au (sehemu nyingine), sijui. Ameshinda kila kitu lakini kamwe hajashinda Ballon d'Or. Nimeshinda mara tatu.”
Straika Messi ameshinda tuzo ya Ballon d'Or mara tano na anatazamwa kama mchezaji bora wa muda wote, lakini Ronaldo anaamini anastahili tuzo hiyo.

Xavi
Akizungumza na Radio ya Hispania mapema wiki hii, Xavi alisema: “Ni mjinga tu ambaye hawezi kutambua kwamba Cristiano (Ronaldo) ni mchezaji bora. Lakini ana bahati mbaya kuzaliwa katika zama sambamba na Leo (Messi).”
Jumamosi Ronaldo alifungia Madrid bao katika dakika ya sita uwanjani Santiago Bernabeu dhidi ya Osasuna na kuifanya kushinda katika mchezo wake watatu wa La Liga.

Messi
Mreno huyo alipondwa baada ya kutoa maoni yake kuhusu Iceland katika michuano ya Euro 2016. Ronaldo alidai wachezaji wa timu hiyo ya taifa wana fikra ndogo baada kushangilia sare dhidi ya Ureno katika hatua ya makundi kama vile wametwaa taji.
Ronaldo pia alida kama angekuwa Rais wa Real Madrid, Florentino Perez, Real, angejipa dili kubwa zaidi Madrid. Mkataba wake wa sasa unaisha mwishoni mwa 2018.


Xavi akiwa Qatar na klabu ya Al Sadd.
Staa huyo aliongeza: “Kama ningekuwa Rais wa Real Madrid, ningejipa mwenyewe mkataba wa miaka 10. Mpaka sasa sifikirii kuhusu kitu kingine kuhusu kazi yangu, kitu ninachotaka ni kustaafu nikiwa Real Madrid. Hii ni klabu kubwa duniani na inapaswa kuwa na wachezaji bora.” 

Post a Comment

 
Top