MANCHESTER,
ENGLAND
JOSE
MOURINHO wa Manchester United,
anafikiria kumpanga kinda Marcus Rashford kwa mara ya kwanza katika pambano linalosubiriwa
kwa hamu duniani kote, lakini bado haijafahamika kama ameamua hivyo.
Rashford
mwenye umri wa miaka 18 tu, Jumanne usiku aliongeza presha kubwa kwa Mourinho
baada ya kufunga ‘hat trick’ katika pambano la U-21 kati ya England dhidi ya
Norway na kumekuwa na kelele za kumtaka aanzishwe katika pambano dhidi ya Man
City.
Kabla
ya hapo, Rashford alikuwa ameiokoa United katika pambano dhidi ya Hull City
akifunga bao la ushindi katika dakika za majeruhi na kuifanya United izoe
pointi zote tisa katika michezo mitatu ya awali Ligi Kuu ya England.
Kinda
huyo amekuwa akifunga kila anapopewa nafasi katika mechi zake za kwanza baada
ya kufunga katika pambano lake la kwanza tu la Manchester United ambalo pia
lilikuwa pambano lake la kwanza la michuano ya Europa dhidi ya Midtjylland
Februari mwaka huu.
Mourinho
Akafunga
tena siku tatu zilizofuata katika pambano lake la kwanza la Ligi Kuu ya England
dhidi ya Arsenal katika ushindi wa mabao 3-2 na hivyo kumfanya awe mfungaji
mwenye umri mdogo zaidi kwa Manchester United katika historia ya Ligi Kuu ya
England baada ya Federico Macheda na Danny
Welbeck.
Kama
vile haitoshi, Rashford alifunga bao lake la kwanza katika siku yake ya kwanza
kuvaa jezi ya timu ya wakubwa ya England katika pambano dhidi ya Australia Mei
mwaka huu kiasi kwamba kocha wa England wa wakati huo, Roy Hodgson aliamua
kwenda naye katika michuano ya Euro iliyofanyika Ufaransa.
Msimu
huu, Rashford amecheza dakika 18 tu katika utawala wa Mourinho kutokana na
nafasi yake kujazwa na mastaa waliojaa klabuni hapo eneo la ushambuliaji, Zlatan
Ibrahimovic, Wayne Rooney na Anthony Martial.
Ibrahimovic
Hata
hivyo, mashabiki wa United wameanza kumpa presha Mourinho ampange kinda huyo
ambaye mwenyewe amedai kwamba mabao yake yatamsaidia kumpa presha Mourinho
kuhusu suala la kumpanga au vinginevyo.
“Hicho
ndicho ambacho anachopaswa kufanya mchezaji mdogo, unampa kocha maamuzi ya
kufikiria akupange au vinginevyo. Nasubiri kwa hamu kucheza,” alisema Rashford
akizungumzia mechi dhidi ya City.
Sio
Mourinho tu, Rashford amemuweka katika presha kubwa kocha mpya wa timu ya taifa
ya England, Sam Allardayce ambaye alimtupa nje kinda huyo katika kikosi chake
cha timu ya wakubwa ambacho kilicheza mechi ya kufuzu dhidi ya Slovakia ugenini
na kushinda bao moja kwa shida katika dakika za majeruhi.
Kocha wa England-Sam-Allardyce.
Kocha
wa kikosi cha England U-21 amedai kwamba hakushangazwa na kiwango cha Rashford na
anaamini kuwa Allardyce atakuwa amemuelewa kinda huyo mzaliwa wa Jiji la
Manchester kufuatia hat trick yake hiyo.
“Haikunishangaza
kabisa. Kitu ambacho tulikiona kwake kwa wiki nzima ndicho tulichokina.
Nisingeweza kuwa na furaha zaidi kuliko kile ambacho alikionyesha. Nitaongea na
Sam siku chache zijazo na nina uhakika kiwango cha Rashford kimemfanya ajifikirie
upya,” alisema kocha huyo baada ya kumalizika kwa pambano dhidi ya Norway.
Post a Comment