Messi
LONDON,
ENGLAND
THIERRY
HENRY anaamini kujiunga kwa kocha, Pep Guardiola Manchester City kutawavutia
wachezaji wenye majina makubwa katika usajili wa mwishoni mwa msimu lakini siyo
Lionel Messi.
Henry
Bosi
huyo wa Bayern Munich atachukua nafasi ya Manuel Pellegrini mwishoni mwa msimu
baada ya kukubali mkataba wa miaka mitatu wenye thamani ya zaidi ya Pauni 15 milioni
kwa mwaka.
Na
Henry ambaye alifundishwa na Guardiola alipokuwa Barcelona, anatarajia kuwa Man
City itakuwa sehemu maarufu zaidi ikiwa chini ya utawala wa Mhispaniola huyo.
“Najaribu
kufikiria atawavutia wachezaji wenye majina makubwa kwa sababu ana vyanzo,
lakini pia hawezi kuogopa kukuza vipaji.
“Pamoja
na kwamba Man City ina academy au vijana wenye vipaji Ulaya ambao hawatakuwa na
gharama kubwa, kama tulivyomuona Kingsley Coman, ambaye mpaka sasa yuko Bayern
Munich.
“Kama
wewe ni shabiki wa Man City, unaweza kuwa na ndoto ya kuwaona baadhi ya
wachezaji wenye majina makubwa. Siyo kwa sababu ni klabu kubwa na ina vyanzo, lakini
Guardiola ni mtu atakayemvutia mchezaji yeyote duniani.”
Awali
Man City ilionyesha kuvutiwa na Messi na kutaka kumpeleka Etihad,
lakini Henry hashawishiki kama mchezaji mwenzake huyo wa zamani wa Barca
anaweza kujiunga na timu hiyo.
Alipoulizwa
kuwa Guardiola anaweza kumshawishi nani kujiunga naye Manchester City, Henry
alisema: “ Labda siyo Messi, lakini wachezaji wengi wanataka kufundishwa na
kocha huyo."
Guardiola
Pamoja
na kwamba klabu iko katika kiwango kizuri, Henry anaamini ubora wa soka utakuwa
bora chini ya Guardiola msimu ujao.
“Pindi
Pep akifika Manchester City, atafika na mawazo yake sahihi,' alisema Henry.
“Naweza
kuwahakikishia kuwa timu itacheza soka katika ubora. Atafika na wachezaji wake
na wengine atawaondoa. Niamini. Alipokuja Barcelona, aliwaondoa baadhi ya
wachezaji. Amefanya hivyo pia Bayern Munich na nadhani atafanya hivyo
Manchester City.
“Kuna
kitu kimoja unatakiwa kuwa na uhakika nacho – atataka kutawala. Kila wakati
atataka kushirikiana na timu yake katika
mabao yatakayofungwa.
“
Kila siku anataka kuwa mbele, kuwa na mpira, kumiliki kama tunavyojua, na
anataka kutawala. Hivyo nawapa hongera, Manchester City.'
Post a Comment