Gurdiola
MANCHESTER,
ENGLAND
PEP
GUARDIOLA ameshathibitishwa kuwa ndiye kocha anayefuata klabuni Manchester City
na atapewa kitita cha Pauni 80 millioni kuwasajili Paul Pogba kwa Pauni 50 milioni, Lewandowski kwa Pauni 75 milioni na beki
wa Everton, John Stones.
Kocha
huyo amekubali dili la kujiunga na Man City la miaka mitatu lenye thamani ya
Pauni 15 milioni na kwa wiki atakuwa akichukua Pauni 40,000 zaidi ya kapteni wa
Manchester United, Wayne Rooney, mchezaji anayelipwa pesa nyingi katika Ligi
Kuu England.
Kocha
huyo Mhispaniola atakuwa akipewa nguvu na matajiri wa mafuta na inaonekana
kuwa mchezaji bora wa dunia Lionel Messi
anaonekana kuwa mbali na mipangilio yao, Man City inataka kuondoa utamaduni wa
wachezaji wakubwa kuhamia Hispania.
Pogba
Guardiola
ambaye amewahi kuzifundisha Barcelona na Bayern Munich, amepoteza michezo 19 tu
kati ya 239 ya ligi na Man City kocha
huyo mwenye umri wa miaka 45 atawavutia wachezaji wenye majina makubwa.
Klabu
za Chelsea, Barcelona na Real Madrid zitashindana kumwania mchezaji wa zamani
wa Manchester United, kiungo Pogba, 22,
ambaye ataondoka Juventus mwishoni mwa msimu na beki Stones, 21.
Lewandowski
Man
City ina matumaini kuwa inaweza kuwarubuni wachezaji hao watakuwa chini ya
kocha wao huyo mpya.
Mbali
na wachezaji hao, Manchester City imejipanga kutoa Pauni 75 milioni
kupambana na Real Madrid kumwania straika wa Bayern Munich Robert Lewandowski.
Madrid
inaamini itamnasa Lewandowski kwa kuwa alionyesha kuitaka klabu hiyo alipofanya
mahojiano na TV ya kwao Poland mapema msimu huu.
Beki wa Everton, Stone (kulia)
Lakini
Man City inafahamu kwamba, Guardiola anayemfundisha Lewy katika miaka yake
miwili Bayern Munich, anaweza kufanya jitihada kumnchukua straika huyo mwenye
umri wa miaka 27.
Kocha
wa sasa wa Man City, Manuel Pellegrini amethibitisha kuwa ataondoka mwishoni
mwa msimu kufuatia mkutano alioufanya kabla ya mechi dhidi ya Sunderland
Jumanne usiku.
Post a Comment