0
Daniel Sturridge
LIVERPOOL, ENGLAND
DANIEL STURRIDGE yuko tayari kuondoka Liverpool  mwishoni mwa msimu kufuatia wapinzani wake kuhoji michango wake katika timu hiyo.
Kocha Jurgen Klopp amesema hadharani kukatishwa kwake tamaa na uwezekano wa Sturridge kuwa fiti na nyota kadhaa wa zamani wa Anfield wameshauri nafasi ya  straika huyo ipate mtu mwingine.

Suarez alipokuwa Liverpool alikuwa na pacha nzuri na Sturridge
Sturridge amechoshwa na mtazamo huo na amemuomba meneja wake amtafutie timu nyingine, kwa sababu wapinzani wake wanaamini hana kiu ya kutimiza majukumu yake katika timu. 
Straika huyo mwenye umri wa miaka 26 amebakisha miaka miwili na nusu katika mkataba wake unaompa Pauni 150,000 kwa wiki, ikimaaanisha Liverpool inaweza kumuuza kwa kiasi kikubwa.
Thamani yake mpaka sasa ni  Pauni 60 miliioni lakini  rekodi yake ya majeraha inaweza kumshusha  hadi kufikia Pauni 20 milioni.
Sturridge bado ana matumaini ya kurudi katika kiwango kilichomfanya kuwa mmoja wa washambuliaji wa kutisha Ulaya. 

Sturridge akiwasili mazoezini, Ijumaa asubuhi
Anapaswa kuthibisha kupona kwake kati ya sasa na mwishoni mwa msimu na kutimiza azma ya Liverpool katika mashindano ya  Kombe la FA, Capital One Cup  na ushindi katika Ligi ya Ulaya (Europa League).
Klabu za Arsenal, Tottenham na Manchester United zitakuwa sokoni kusaka mastraika wapya mwishoni mwa msimu.  
Arsenal ilionyesha nia ya kweli kumtaka Sturridge Januari 2013, lakini wakati wakijadiliana kuhusu dau lake, straika huyo akajiunga Liverpool f akitokea Chelsea kwa Pauni 12 milioni.
Sturridge ameumia kila kiungo.

Sturridge anaweza kucheza katika klabu yoyote ya Ulaya lakini mwenyewe anapendelea kubaki Ligi Kuu England.
Mwaka 2014 aliongoza mashambulizi ya England katika Kombe la Dunia 2014  na kocha Roy Hodgson alimsifu kuwa ni straika wa kawaida aliyebarikiwa.
Mwezi Novemba, Klopp alisema: “ Tunatakiwa kukubali kwamba Danny  kila mara amekuwa majeruhi katika miezi ya hivi karibuni, labda miaka.
“Ukiwa na Danny unapaswa kujifunza aina mpya ya ukali mazoezini na unatakiwa kujifunza kuhusu maumivu makali na maumivu ya kawaida.”
Wachezaji wa zamani wa Liverpool wakiwemo Dietmar Hamann na Phil Thompson wameshauri timu hiyo itafute straika mwingine mpya.



 

Post a Comment

 
Top