0


Ed Woodward
MANCHESTER, ENGLAND

ED WOODWARD Makamu Mwenyekiti wa Manchester United anatarajiwa kuwekwa kiti moto wiki ijayo katika mjadala wa maendeleo ya timu hiyo likiwemo suala la kuendelea kwa kibarua cha kocha, Louis Van Gaal.

Makamu Mwenyekiti huyo wa Man United atatakiwa kuandaa mkutano na wawekezaji Alhamisi kwa njia ya simu kujadili maendeleo ya robo ya mwisho wa msimu huu.

Kocha Van Gaal amekuwa katika presha kubwa kutokana na kiwango kibovu na matokeo mabaya kwa timu hiyo ya Old Trafford ambayo imetolewa kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya mwezi Desemba.

Man united kwa sasa iko katika nafasi ya nne Ligi Kuu England na nje ya Ligi ya Mabingwa Ulaya japokuwa Jumanne usiku iliifunga Stoke City mabao 3-0.


Gigs akiwa na Van Gaal
Woodward alipinga alipotakiwa kumpigia simu ya kumfukuza kazi kocha Van Gaal mwenye miaka 64 lakini presha imekuwa kubwa kufuatia wapinzani wao, Manchester City  kumwajiri kocha, Pep Guardiola ambaye anatarajiwa kuanza kazi mwishoni mwa msimu huu.

Na Woodward atatakiwa kutoa majibu juu ya athari za kifedha kwa United kufuatia kushindwa kufuzu mashindano ya Ulaya kwa mara ya pili ndani ya misimu mitatu.

Pia, inafahamika kwamba Man United imewaandikia barua mashabiki wake  kuwaomba kuwaunga mkono katika Ligi ya Ulaya (Europa League) watakapopambana na FC Midtjylland baadaye mwezi huu.


Post a Comment

 
Top