0
Chicharito
COLOGNE, UJERUMANI

JAVIER HERNANDEZ ‘Chicharito’ amesisitiza asingeondoka Manchester United kama Louis van Gaal angemwahidi kucheza lakini straika huyo amedai hakuwa tayari kukalia benchi.
 Chicharito mwenye umri wa maika 27 alijiunga na Bayer Leverkusen  kwa Pauni 7.3 milioni  Agosti mwaka jana  na amefunga mabao 13 katika michezo 16 ya  Ligi ya Bundesliga msimu huu.

Mashabiki waliniambia nibaki
Straika wa kimataifa wa Mexico aliambiwa na Van Gaal kwamba atakuwa akicheza badala ya Wayne Rooney na hakuwa na chaguo lingine zaidi ya kuondoka.
“Kama angeniambia miye ni  straika namba moja nisiweza kuondoka,” Hernandez aliliambia  Gazeti la The Times.  “Lakini nilihitaji kucheza.”
“Nilikuwa kwa ajili ya timu kwa miaka mitatu. Niliangali jinsi ya kuwa pale, kufanya kazi na kuishi vizuri na wachezaji wenzangu na nilikuwa tayari. [Ilikuwa ni wakati huo]  baadaye nikataka kujiangalia mwenyewe, kuangalia malengo yangu.
“Mashabiki walitaka niendelee kubaki lakini nibaki kama mchezaji wa akiba. Sikutaka kubaki zaidi. 
“Nilirahisi kusema hutaki kufanya mazoezi, kuchati au kuweka picha katika Mtandao wa Instagram kwa sababu huchezi, huko sasa ni kutaka kugombana na kocha.”

akishangilia bao
Hernandez alisema hana kinyingo na dhidi ya Van Gaal, kwa sababu alimwambia ukweli.
“Alikuwa ni mkarimu,” straika huyo aliendelea kusema: “ Kwenye wiki za mwanzo, aliniambia anauona wakati wangu mzuri mbele ya safari, kwamba nitakuwa na nafasi kubwa ya kucheza kuliko kawaida. Nikajua nitapata muda wa kucheza. 
“Lakini baada ya kuanza kwa msimu, aliniambia anadhani Wazza atakuwa namba 1wake.”
Hernandez ataiongoza Leverkusen Jumamosi hii katika mchezo wa Ligi ya Bundesliga dhidi ya Bayern Munich katika uwanja wa nyumbani. 
 

Post a Comment

 
Top