0
Jose Mourinho hakutaka kupewa kazi katikati ya msimu.
LONDON, ENGLAND

JOSE MOURINHO ananukia kupata kibarua cha ndoto yake na anatarajia kuwa kocha wa Manchester United mwishoni mwa msimu.
Imekuwa ni wiki ya kishindo kwa Manchester, baada ya kutangazwa kwa Pep Guardiola kuwa ataanza kuinoa Man City mwezi wa Julai, na sasa bila ya shaka  watataka kudumisha upinzani wao kwa  Man United kujipanga kumpa kazi Mourinho.

Upinzani huu unatarajiwa kujirudia England
Hakuna dili lililofanyika mpaka sasa lakini Mourinho ameupanga moyo wake kuipata kazi hiyo.
Kocha huyo aliyefukuzwa Chelsea ameweka wazi kwamba  anataka kuendelea kufanya kazi Ligi Kuu England na amekataa ofa mbili  za kurudi Hispania kuifundisha Real Madrid.

Kombe la tatu.
Ofa ya kwanza ilikuwa ni kabla ya Rafa Benitez kuchaguliwa kuwa kcoha mwishoni mwa msimu uliopita,  na nyingine  baada ya kocha huyo kufukuzwa Chelsea in Desemba –  kwa hiyo ataendelea kubaki England.
Mourinho alitajwa na Sir Alex Ferguson mwaka 2013 kwamba angeweza kuwa mrithi wake lakini alikuwa tayari ameshajifunga kuitumikia Chelsea wakati alipojuwa kuwa anaondoka Bernabeu.
Nafasi hiyo kwa Louis Van Gaal imekuwa imezidi kuwa ngumu msimu huu, kutokana na Man United ikijitahidi kupigania kuwepo katika Top Four na wakipanga kufanya mabadiliko mwishoni mwa msimu.
Akiteta na Ferguson.

Chanzo cha karibu ya Mourinho kimesema kuwa kocha huyo alikataa kukinoa kikosi hicho cha Old Trafford katikakati ya msimu, akipendelea zaidi kuanza upya  msimu wa 2016/17. 
Bosi huyo wa zamani wa Inter Milan na Real Madrid ameiongoza Chelsea kushinda taji  lake la tatu la Ligi Kuu msimu uliopita, kabla ya kufukuzwa kwa mara ya pili katika klabu hiyo.

Van Gaal ataaga mwishoni mwa msimu.
Hata hivyo, uvumi uliotawala ni kuwa machafuko katika kikosi cha Chelsea ulitokana na utata wa sakata la daktari Eva Carneiro.
Kikosi hicho cha Mourinho kimekuwa na wakati mgumu kwa kuanza msimu vibaya na kuonekana kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wao hadi alipofukuzwa Desemba. 

 

Post a Comment

 
Top