Di Maria akifanya vitu vyake PSG.
PARIS, UFARANSA
MCHEZAJI wa zamani wa Manchester
United, Angel di Maria amefafanua wakati wake akiwa Old Trafford kama ‘uzoefu
wa kusikitisha’ na hataki kuukumbuka.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina
alisajiliwa kutoka Real Madrid kwa usajili ambao ulivunja rekodi England wa
Pauni 59.7 milioni Agosti 2014.
...akipachika bao
Di Maria alianza kwa nguvu lakini
baadaye alipotea vibaya kabla ya kuuzwa dau
linalodaiwa kuwa Pauni 44 milioni kwa mabingwa wa Ligi 1, Paris Saint Germain
mwishoni mwa msimu uliopita.
Di Maria alijitahidi kukaa sawa
baada ya jaribio la wizi nyumbani kwake Manchester
kabla ya kuingia katika ugomvi na kocha Louis
van Gaal na kukiri kwamba wakati wake akiwa Ligi Kuu haukuwa kama alivyopanga.
Akizungumza na Gazeti la L’ Equipe, Di
Maria mwenye umri wa miaka 27 alisema: “Manchester nilipata uzoefu wa
kusikitisha sana. Mambo hawakwenda kama nilivyotarajia, nilikata tamaa na
sikutarajia.
...alipojiunga na Man United.
“Kwa kweli, sikumbuki nini kilitokea na sitaki kukumbuka,”aliongeza.
Baada ya kufunga mabao manne katika michezo 32 akiwa na Man United, Di Maria amerudisha kiwango chake akiwa Paris – kwa kufunga mabao manane na kutoa pasi zilizozaa mabao10 kwa vinara hao wa Ligue 1 ambao wanatarajiwa kukutana na Chelsea katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Baada ya kufunga mabao manne katika michezo 32 akiwa na Man United, Di Maria amerudisha kiwango chake akiwa Paris – kwa kufunga mabao manane na kutoa pasi zilizozaa mabao10 kwa vinara hao wa Ligue 1 ambao wanatarajiwa kukutana na Chelsea katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Pamoja na kiwango kibovi
alichoonyesha katika Ligi Kuu England, Di Maria amesisitiza kwamba hana cha kuthibitisha
ubora wake dhidi ya Chelsea ili kuifikisha PSG katika fainali ya Ligi ya
Mabingwa msimu huu.
Post a Comment