Vidal
akiwa Qatar na mashabiki wake.
MUNICH, UJERUMANI
KIUNGO
wa Bayern Munich, Arturo Vidal ametishia kuchukua hatua za kisheria Gazeti la
Bild la Ujerumani baada ya kuchapisha taarifa kwamba alifika mazoezini akiwa
amelewa.
Gazeti hilo liliripoti kwamba Vidal
raia wa Chile aliondoka kambini iliyowekwa Qatar katika majira ya baridi na
kwenda kwenye mambo yake binafsi mwezi
Januari na alirudi akiwa amekolea kwa kinywaji.
Lakini Vidal alikanusha madai hayo
na kusema ni ya uongo kwa kutumia akaunti yake ya Mtandao wa Instagram.
“Napenda kusema kwamba habari zilizochapishwa leo katika Ujerumani bila shaka si za kweli. Wanasheria wangu tayari wanaandaa madai dhidi ya gazeti na watawajibika kwa kuandika uongo,” aliandika Vidal.
“Napenda kusema kwamba habari zilizochapishwa leo katika Ujerumani bila shaka si za kweli. Wanasheria wangu tayari wanaandaa madai dhidi ya gazeti na watawajibika kwa kuandika uongo,” aliandika Vidal.
“ Kwa asilimia 100 nilikuwa
karibu na timu yangu na kujiandaa kwa hatua ya kumalizia msimu jambo
ambalo ni muhimu kwetu sote.
Gari ya Vidal ilipopata ajali“Asante kwa klabu yangu kuniunga mkono na asante kwa mashabiki wangu kwa kila siku kuonyesha kwamba wananipenda.”
Mwenyekiti wa Bayern Munich, Karl-Heinz
Rummenigge alitoa maoni yake: “Tuhuma zote ni uongo mtupu.''
Vidal alijiunga na Bayern Munich
akitokea Juventus mwishoni mwa msimu uliopita na amefunga mabao matatu katika
michezo 28 aliyoitumikia timu yake katika Ligi ya Bundesliga.
Mchezaji huyo mwishoni mwa
msimu uliopita alitengeza vichwa vya
habari wakati wa michuano ya Copa
America baada ya kupata ajali ya gari lake aina ya Ferrari.
Post a Comment