0


MADRID, HISPANIA
MAELFU ya mashabiki wa Real Madrid  wamempokea Zinedine Zidane katika mazoezi kiwanjani Valdebebas kwa mara ya kwanza baada ya kuchaguliwa kuwa kocha wa timu hiyo.

Zidane mazoezini
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 43 ametangazwa kuchukua nafasi ya Rafa Benitez katika klabu hiyo jana Jumatatu.
Kocha huyo Mfaransa anaiandaa timu  kwa ajili ya mechi ya kwanza dhidi ya timu iliyoko katika nafasi ya saba, Deportivo la Coruna Jumamosi katika  uwanja wa nyumbani wa Bernabeu.



Zidane kulia akiongoza mazoezi
Katika mazoezi hayo, Zidane  hakuwa na straika, Gareth Bale, huku ikiaminika straika huyo alikuwa akifanya mazoezi ya ‘gym’ nje ya timu. 
Bale anahusishwa na kuondoka katika timu hiyo  na kurudi England, baada ya kuondoka kwa Benitez.
Kwa mara ya kwanza,katika mazoezi hayo  kinda, Mnorweyi, Martin Odegaard kutoka timu ya vijana ya Madrid, Castilla alicheza.

 Zidane
Zidane
Kikazi zaidi
 Ronaldo na beki Nacho Fernandez
 Zidane




Post a Comment

 
Top