0


MADRID, HIPASNIA
KOCHA wa Real Madrid, Rafa Benitez amefukuzwa kazi baada ya miezi saba ya kuinoa timu hiyo na Zinedine Zidane ametangazwa kuchukua nafasi yake.
Wakati wa kufanya uamuzi ulifika na miamba hiyo ya  Hispania iliitisha kikao cha dharula  baada ya Real Madrid kutoka sare na Valencia Jumapili jioni.

Zidane
Rais wa Madrid, Florentino Perez alifanya uamuzi huo baada ya timu hiyo kushika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi, ikiwa pointi mbili nyuma ya wapinzani wao, Barcelona na nne kwa vinara, Atletico Madrid.
Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Jumatatu baada ya kutangaza uamuzi huo, Perez alisema: “Bila shaka Rafa Benitez ni mtaalamu na mtu wa ajabu. Tumeamua kumchagua Zinedine Zidane kuwa kocha mpya wa Real Madrid.”

Zidane na Perez
Akimtambulisha Zidane, Perez alisema : “ Hii ni klabu yako, huu ni uwanja wako. Na una baraka zetu zote. Kutoka muda huu wewe ni kocha wa Madrid.
“Najua neno  ‘haiwezekani’ haliishi katika fikra zako.” 
Hata hivyo, Perez anabaki kuwa shabiki mkubwa wa kocha wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho.

Akizungumzia jukumu hilo, Zidane, ambaye alishinda Ligi ya La Liga na Ligi ya Mabingwa wa Ulaya akiwa mchezaji wa timu hiyo, alisema: “Hii ni klabu nzuri duniani na yenye ngome ya mashabiki duniani kote. Nataka kuhakikisha kwamba mwishoni mwa msimu klabu hii itakuwa na kombe. 
“Nitafanya kazi kwa bidii na wachezaji wote na nadhani mambo yatakwenda vizuri. Kesho ndio kazi itaanza. Nitajitoa kwa moyo wangu wote kwa klabu huu, asanteni.”

 Benitez
Michezo minane ambayo Benitez hajapata ushindi Madrid:  
Agosti 23 – Sporting Gijon 0-0 Real Madrid.
Septemba 26 – Real Madrid 0-0 Malaga.
Oktoba 04 – Atletico Madrid 1-1 Real Madrid.
Oktoba 21 – Paris St Germain 0-0 Real Madrid.
Novomba 08 – Sevilla 3-2 Real Madrid.
Novemba 21 – Real Madrid 0-4 Barcelona.
Desemba 13 – Villarreal 1-0 Real Madrid.
Januri 03 – Valencia 2-2 Real Madrid.

Post a Comment

 
Top