TURIN,
ITALIA
MANCHESTER UNITE KIUNGO wa Ufaransa, Paulo
Pogba amesema muda aliokuwa Manchester
United ni sawa na kama alikuwa likizo akilinganisha na kiwango cha juu
alichokuwa nacho katika Ligi ya Serie A
na Juventus.
Pogba
aliondoka Old Trafford mwaka 2012 akiwa
amecheza katika kikosi cha kwanza mara tatu chini ya Sir Alex Ferguson.
Mara
baada ya kuondoka Ligi Kuu England, Pogba ameisaidia Juventus kwa kuipa mataji
mara tatu.
POGBA
“Watu
wanatakiwa kujua kuwa hakuna kitu rahisi Juve,' Pogba aliiambia gazeti la
Italia la Stampa.
“Kuna
utamaduni tofauti wa kazi ukilinganisha na sehemu nyingine. Nilikuwa Manchester
na ilionekana kama nilikuwa likizo.
“Hapa
tunafanya kazi zaidi. Haya mataji yote hatukuyaiba. Ilikuwa ni kazi mwanzo
mwisho.”
Pogba
ambaye anahusishwa kuhamia katika timu za Barcelona, Manchester City na Chelsea
miezi michache ijayo alipigwa picha akiwa na Mario Balotelli Jumapili jioni.
Wakala
wa Balotelli, Mino Raiola ndiye pia anayemwakilisha Pogba anapanga kufanya
mazungumza na Kocha wa Liverpool, Jurgen Klopp kumshawishi kumpa nafasi
nyingine Balotelli ndani ya Anfield.
POGBA alipokuwa Man United.
Akizungumzia
tetesi za usajili wake, Pogba alisema yeye si kitu pamoja na kwamba anaangaliwa
na timu yenye hadhi kubwa na inayompa maendeleo.
“Katika
historia jezi ya Juve ni muhimu na nataka kuipa heshima. Pindi ninapoingalia jezi sioni namba wala jina
langu, kitu pekee ninachokiona ni Juve na kuwa na tamaa ya kujitoa kwa asilimia
100 na kushinda,” alisema Pogba.
POGBA akiwa na Balotelli
“
Mimi siyo kitu kwa kweli, sijafanya kitu katika kazi yangu.”
Post a Comment