0


VALENCIA, HISPANIA
MCHEZAJI wa zamani wa Manchester United, Gary Neville amesema anadhani ataendelea kuinoa  Valencia msimu ujao baada ya jana Jumapili kutoka sare ya mabao 2-2 na Real Madrid.
Neville ambaye ana mkataba wa miezi sita na timu hiyo, hivi karibuni alikaririwa  akisema hatakuwa na muda mrefu katika kufanya kazi ya ukocha.

Lakini baada ya sare hiyo na Real Madrid alisema: " Nilikuwa naamanisha kuhusu miaka 15 hadi 20  nilipozungumzia kuhusu  kendelea  na uongozi.
" Kwa hakika niko hapa kwa miezi sita lakini ninataka kujihakikisha maisha ya baadaye."
Beki huyo wa zamani wa Manchester United amevuna pointi tatu katika michezo minne  ya Ligi ya La Liga mpaka sasa.
Timu yake imeizuia Real Madrid ambayo ni moja kati ya timu inayofukuzia ubingwa ikiwa katika kiwango bora, kwa mchezaji Paco Alcacer kusawazisha bao dakika za lala salama.
“Jambo la faraja  ni kuiona timu ikiwa fiti, ina nguvu, inapiga pasi vizuri na tunaokena tuko vizuri katika upande wa beki. Kuna vitu vinavyofanyika na ninaviamini. Ni kiwango bora mpaka sasa,” alisema Neville.

Post a Comment

 
Top