SOUTHAMPTON, ENGLAND
MAISHA ya baadaye ya Straika Sadio
Mane ndani Southampton yameingia katika shaka baada ya kuadhibiwa na kocha wake
Mholanzi, Ronald Koeman kutokana na kuchelewa kufika katika mkutano wa klabu.
Southampton
iko tayari kukubali kumuuza mchezaji huyo Manchester United anayelipwa kwa Pauni 125,000 kwa wiki kwa dili la miaka
mitano.
Ada ya Pauni 30 millioni itakuwa ya kushtua kumpeleka Old Trafford ambapo kocha Louis Van Gaal, anahitaji kuongeza nguvu ya ushambuliaji kwa kumuonge na Felipe Anderson wa Lazio.
Mane, late for a team meeting ahead of Saints’ 1-0 loss at Norwich yesterday, wants a big move.
Kocha wa Manchester United, Louis
Van Gaal kukiri kumfuatilia kwa karibu Msenegali huyo.
Mane alichelewa katika mkutano wa
timu kwa saa mbili kabla ya mchezo dhidi ya Norwich na Kocha Koeman alimwadhibu
kwa kumuondoa katika kikosi cha kwanza.
Kocha Koeman alishazungumza na Mane kuhusu
ukosefu wa umakini katika mazoezi Alhamisi iliyopita na tukio hili la sasa linaashiria
kuwa ataondoka Januari.
Bosi huyo wa Southampton hajasema
kama atampiga faini mchezaji huyo, lakini amemshutumu kwa kuwaangusha wachezaji
wenzake na mashabiki kutokana na kutokuwepo kwake.
“ Tuna vikosi tofauti kwa ajili ya
mechi. Alikuwa mmoja wa wachezaji 11waliotakiwa
kuanza, lakini tuna sheria katika timu yetu. Amefanya kosa kubwa sana.
“Simwelewi mchezaji anayekuja akiwa amechelewa kwenye mkutano wa mwisho. Nadhani hakuupokea na kuuzingatia ujumbe wangu wa Alhamisi.’
“Simwelewi mchezaji anayekuja akiwa amechelewa kwenye mkutano wa mwisho. Nadhani hakuupokea na kuuzingatia ujumbe wangu wa Alhamisi.’
Koeman
alisema: “Klabu inamheshimu kila mmoja, ana majukumu kama mchezaji kwa
mashabiki, kwa wenzake, kwa bodi na kwa benchi la ufundi na hii inaumiza sana.”
Hii ni mara ya pili kwa Mane
kuadhibiwa kwa kosa kama hilo. Alifika
akiwa amechelewa katika mkutano wa mchezo wa nyumbani dhidi ya Liverpool msimu
uliopita.
Kocha huyo alikatishwa tamaa na kitendo hicho ambacho kimetokea siku moja baada ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ralph Krueger kuwatakia wachezaji heri ya mwaka mpya, na kuzumgumzia molari ya timu, nidhamu, malengo na matarajio.
Kocha huyo alikatishwa tamaa na kitendo hicho ambacho kimetokea siku moja baada ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ralph Krueger kuwatakia wachezaji heri ya mwaka mpya, na kuzumgumzia molari ya timu, nidhamu, malengo na matarajio.


Post a Comment