MADRID,
HIPSANIA
CRISTIANO
Ronaldo amebainisha kwamba hataki kuendelea kuwepo katika soka baada ya
kustaafu zaidi ya kuishi kama mfalme
Straika
huyo wa Real Madrid, ambaye mwezi ujao atafikisha umri wa miaka 31, anaamini ni
vigumu kwake kuachana na mchezo huo ghafla lakini anataka kufurahia maisha na
marafiki na familia yake baada ya kustaafu.
“Kuna
maisha mengine badala ya mchezo wa mpira wa miguu,” Ronaldo alisema.
“Nadhani mara ya kwanza itakuwa vigumu, lakini umeniuliza kama nitataka kuwa kocha, naweza kusema hapana. Sitaki kuwa kocha wala rais wa klabu.
“Ukiwa
kocha unaweza kusema kuwa una kazi nzuri, pesa, magari, nyumba...lakini hivyo
siyo kila kitu. Mfano: Jumamosi moja kutakuwa na pambano la ngumi Las Vegas na
nataka kuichukua familia yangu na marafiki kwenda, lakini sitaweza kwa sababu
sitakuwa na nafasi.
“Lakini
baada ya kuachana na soka nataka kuishi kama mfalme. Nimekuwa nilivyo leo kwa
sababu ya muda nilioutumia bila ya familia yangu na kupitia wakati mgumu.
“Nilikuwa
kijana mdogo lakini nililazimika kufanya mambo kama mtu mzima – kujipigia pasi
(nguo) mwenyewe. Nguvu ya akili yangu ilianza kutumika wakati huo.”
Ronaldo alipokuwa na Neville, Man United
Ronaldo
anajiandaa kwa mchezo wa Madrid dhidi ya Valencia Jumapili hii uwanjani
Mestalla. Valencia inafundishwa na
mchezaji mwenzake wa zamani wa Manchester United, Gary Neville.
Madrid
kama itashinda mchezo huo itafikisha pointi 39 sawa na Barcelona, baada ya timu
hiyo inayofundishwa na Luis Enrique kutoka sare ya 0-0 na Espanyol Jumamosi.
Post a Comment