SUNDERLAND, ENGLAND
INGEKUWA Bongo wala watu wasingeshangaa.
Kingeonekana ni kitendo cha kaiwada tu, lakini kimetokea katika Ligi Kuu
England inayoheshimika na wengi.
Kocha wa Aston Villa, Remi Garde
amekataa kupeana mikono na mwenzake wa Sunderland, Sam Allardyce kufuatia
kipigo cha mabao 3-1 ilichokipata timu yake ugenini.
Kocha Garde kushoto akikataa kusalimana na kocha Sunderland.
Pamoja na kipigo hicho katika Ligi
Kuu England, Garde anaweza kukumbana na adhabu kwa kupigwa faini baada ya
kukacha kuzungumza muktasari wa mchezo huo kwa waandishi wa habari.
Kutokana na kipigo hicho wachezaji wa Villa
walisumbuliwa na mashabiki wao wakati wakienda kupanda basi nje ya Uwanja wa Light.
Makocha wakizozana
Villa haijapata ushindi katika
michezo tisa ikiwa chini ya kocha Garde na
wacheza kamali wa naipa timu hiyo nafasi ndogo ya kufanya vizuri.
Kocha huyo Mfaransa alinaswa
akikataa kupeana mkono na mwenzake Allardyce na wakati wa mahojiano ya TV alisema:
“Ningefurahi kama kocha Allardyce angekuja mapema kabla ya mchezo na
kunisalamia.
Timbwili likiendelea
“Nadhani ilikuwa ni rahisi kwake
kuja baada ya mchezo na kusema ‘hongera’. Lakini katika kuonyesha ishara ya kukaribisha alitakiwa kuja mapema,
lakini sikujali kuhusu jambo hilo. Nilichanganyikiwa na matokeo.”
Kocha Garde
Akiuzungumzia mchezo huo, Garde
alisema: “Ni masikitiko makubwa, kama kipigo kingine.
“Sijakata tamaa, kusema kweli. Ninajaribu
kufanya kazi yangu kwa ubora kadiri ninavyoweza kila siku na kila dakika.”
Post a Comment