0


MANCHESTER, ENGLAND
KOCHA Louis van Gaal amemsifu staa wake Wayne Rooney na kusema kwamba kuanzia sasa mchezaji huyo atakuwa mshambuliaji wake mkuu katika kikosi kipya cha Manchester United.
Van Gaal pia alimsifia Rooney kwa uwezo wake wa kukaba akizuia mashambuliaji wa Swansea City kabla ya kufunga bao la ushindi kwa kisigino. Rooney alihusika pia kwenye bao la Anthony Martial baada ya kuingia krosi ya Ashley Young na kuwazuga mabeki wa timu pinzani.
Van Gaal alisema: “Siku zote nimekuwa nikimwambia awe anakimbilia golini, amefanya hivyo na kumpa Martial nafasi ya kufunga na kisha akafunga bao zuri sana kwa mguu wa kushoto, akifanya hivyo kwa kisigino. Huwezi kulifikiria bao kama lile kwamba litafungwa.”

Wayne Rooney akifunga bao la ushindi.
Bao hilo la Rooney ni la 238 tangu alipojiunga na Man United na hivyo kumpiku Denis Law katika orodha ya wafungaji bora wa muda wote wa timu hiyo. Amebakiza mabao 11 kumfikia 11.
Rooney pia amempiku Andy Cole na kushika nafasi ya pili kwa ufungaji kwenye Ligi Kuu England baada ya kufikisha mabao 188, mabao 72 nyuma ya kinara Alan Shearer.
Van Gaal alisema amefurahishwa na Rooney kutokana na kuonyesha kiwango kizuri katika mechi mbili za karibuni ikiwamo ile dhidi ya Chelsea.
Kocha huyo raia wa Uholanzi alisema kwamba timu yake kwa sasa anaitambua kama Man United mpya kutokana na kubadili mfumo wa kiuchezaji, ambapo sasa atabaki na mabeki watatu tu na wengine wote wanakwenda mbele kushambulia.


Post a Comment

 
Top