0


                                 MANCHESTER, ENGLAND
MANCHESTER UNITED imeripotiwa kujipanga kumpa kocha wake, Jose Mourinho mkataba wa mpya wa miaka mitano wenye thamani ya Pauni 65 million, na Mreno huyo yuko tayari kusaini.
United imevutiwa na utendaji kazi wa Mourinho Old Trafford tangu alipomrithi Louis van Gaal Mei 2016 na dili lake jipya litaendelea kumlipa mshahara wa zamani wa Pauni 250,000 kwa wiki ila bonasi zake zitaongezeka mara dufu.
Mourinho, 54, alisaini mkataba wa miaka mitatu na Mashetani Wekundu hao, na atapewa ofa hiyo baada ya kuwa na mwanzo mzuri  katika msimu wa 2017-18, ambapo kikosi chake kiko nafasi ya pili katika Ligi Kuu, nyuma ya Manchester City kwa tofauti ya bao moja.
Pia, Mourinho anavuna matunda yake ya msimu uliopita bada ya kuisaidia Manchester United kutwaa mataji mawili ya Kombe la EFL na lile la Europa League.  Taji la Europa League liiisaidia United kurudi katika Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na kwamba ilimaliza nafasi ya sita katika Ligi Kuu.
Kocha Mourinho amekuwa akipata mafanikio makubwa katika kazi yake lakini ni amekuwa na sifa ya kukaa kwenye klabu kwa muda mfupi.
Muda mrefu aliitumia alipojiunga  kwa mara ya kwanza  na Chelsea kabla ya kufukuzwa. Alichaguliwa katika msimu wa 2004-05, na kushinda mataji mawili ya Ligi Kuu  ndani ya miaka mitatu aliyokaa Stamford Bridge kabla ya kuondoka mapema katika msimu wa 2007-08. 
Mourinho alikaa miaka miwili na nusu na FC Porto na miaka miwili na Inter Milan na kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na timu hizo.
Misimu mitatu kabla ya kutimuliwa Real Madrid, alivunja utawala wa wa miaka mitatu ya Barcelona kutwaa taji la La Liga kwa kuipa timu yake ubingwa wa Hispania  msimu wa 2011-12. Kwa dili hilo jipya la United kuwekwa mezani, Mourinho anajipanga kuwa kocha wa muda mrefu wa klabu hiyo.

Anaonekana ameweza kurithi vyema mikoba ya watangulizi wake, David Moyes na Van Gaal na kuifanya United kuwa na uhai kwa mara nyingine.

Mabosi na mashabiki wa United hawatakuwa na matatizo na Mourinho Old Trafford kama ataendelea kutwaa mataji, bila shaka  na lile taji la Ligi Kuu. 

Post a Comment

 
Top