0


                       PARIS, UFARANSA
EDINSON CAVANI (picha chini) na Neymar wameingia katika vita kubwa na kuna ripoti mpya zinazofichua kisa cha Cavani kumnyang’anya mpira Neymar wakati akitaka kupiga penalti katika mchezo wa Ligue 1 dhidi ya Lyon.
Wawili hao walionekana wakizozana kwa muda mrefu wa mchezo huo uliopigwa Jumapili usiku, huku Cavani akikataa kumwachia majukumu hayo mchezaji mwenzake huyo mpya.
Baada ya mchezo huo, Neymar na Cavani walikaribia kupigana walipokuwa katika vyumba vya kubadirishia nguo, na Neymar akamfuta Cavani katika mitandao yake ya kijamii ya Twitter na Instagram.
Kwa mujibu wa Gazeti la L’Equipe, sababu ya Cavani kutaka kupiga penalti za PSG na kutaka kuwa Mfungaji Bora wa kikosi hicho na kuvuna bonasi ya Uero1 million.
Inaaminika straika wa zamani wa PSG, Zlatan Ibrahimovic alikuwa akipata bonasi kwa kuwa alikuwa na kifungu hicho katika mkataba wake na PSG, ndio maana alikuwa nyuma ya adhabu zote za mipira iliyokufa za timu hiyo kabla ya kuhamia Manchester United.

Ripoti hiyo haikuthibitisha kama Neymar ameingia makubaliano kama hayo na PSG au la, lakini inaaminika kuwa anaweza kuwa nayo.

Kwa sasa Cavani anaongoza katika chati ya ufungaji ndani ya PSG baada ya kufunga mabao saba katika michezo sita ya ligi, wakati Neymar akifuatia kwa kuwa na mabao manne katika michezo mitano hadi sasa.

Post a Comment

 
Top