0


                            MADRID, HISPANIA
DIEGO COSTA atashuhudia mchezo wa timu zake mbili, Chelsea na Atletico Madrid uwanjani Wanda Metropolitano jijini Madrid, akiwa jukwaani.
Pia, staa huyo ataruhusiwa kutembea katika njia wanayopita wachezaji wanapotoka vyumbani na kupata fursa ya kusalimina nao.
Kisha atapanda jukwaani lakini habari kutoka Hispania zinasema hatarajiwi kuingia mbele ya uwanja na kuonekana na mashabiki kama anavyotaka Kocha Simeone ili aweze kuzingatia mechi hiyo. 
Matukio hayo yanakuja baada ya   Jumanne usiku kukamilika rasmi kwa dili lake la kurudi Atletico Madrid akitokea Chelsea baada ya pande timu hizo mbili kukubaliana.
Dili la uhamisho la Pauni 58 milioni litatolewa Januari huku staa huyo wa kimataifa wa Hipsania akijaandaa kurudi tena mikononi mwa kocha wake, Diego Simeone.
Straika huyo mwenye umri wa miaka 28- amesaini uhamisho wa mkopo hadi mwishoni mwa msimu, pamoja na Atletico kuzuiwa kufanya uhamisho ikimaanisha hatacheza hadi Januari. Kisha dili hilo litakuwa la kudumu hadi usajili wa majira ya joto.

Uhamisho wake utakuwa wa mkopo hadi Januari.
Atletico itamlipa Costa mshahara wote wa Pauni 150,000 kuanzia sasa hadi majira ya joto ambapo imekubalika kuwa ndio utafanyika uhamusho wa kudumu.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania atavaa jezi No18 akiwa katika mavazi ya Wanda Metropolitano.
Diego Costa, amefunga mabao 59 katika michezo 120 akiwa Chelsea – Ameshinda taji la Ligi Kuu mara mbili na Kombe la Ligi, ana furaha kurejea katika Mji Mku wa Hispania.

Costa akishuhudia mchezo wa Atletico dhidi ya  Sevilla.
“Nina furaha kurejea nyumbani, kila siku nimekuwa nikisema hivyo, Atletico ni nyumbani, nina furaha, nimefurahi sana,” alisema mara baada ya kujiunga na Altetico Madrid.
“Ningalia mbele kuanza kutoa mchango wangu. Ninatarajia kujitoa kwa nguvu zangu zote kwa ajili ya timu, kama siku zote nilivyokuwa nikijaribu kufanya.
“Juhudi maalumu zilizofanywa na Miguel Angel Gil (Mkurugenzi Mkuu wa Atletico), na klabu nzima kwa jumla kwa kukamilisha uhamisho huu, nina furaha na kila mmoja.” 
Costa alimaliza misimu mitatu akiwa mfungaji bora wa klabu wa kila msimu alipokuwa Stamford Bridge baada ya kununuliwa kwa dili la Pauni 32 milioni akitokea Atletico Julai 2014.

Enzi zake akicheza dhidi ya Chelsea.
Hata hivyo, kukosana kwake hadharani na Kocha wa Chelsea, Antonio Conte majira ya joto ilimaanisha mwisho wake haukuwa mwema Magharibi mwa London.
Pia, mabingwa hao wa Ligi Kuu England wamemtakia heri kufuatia kuondoka kwa Costa: “Tunamshukuru Diego kwa jitihada zake na tunamtamka kila la heri.”

Post a Comment

 
Top