BARCELONA, HISPANIA
BARCELONA imewasilisha
ofa mpya ya Uero125 milioni (Pauni 114.2 milioni) ili kumnasa kiungo wa
Liverpool Philippe Coutinho.
Hata hivyo, Liverpool
imeikataa ofa hiyo kutoka kwa miamba hiyo ya La Liga na kuendelea na msimamo kuwa
nyota huyo hauzwi.
Barcelona inataka
kumnyakua staa huyo wa kimataifa wa Brazil baada ya kumuuza Neymar kwenda PSG kwa
ada ilivyovunja rekodi ya dunia na imekubali kulipa kiasi kikubwa zaidi ya Euro130
milioni (Pauni118.7m) kumpeleka Coutinho Nou Camp.
Bosi wa Liverpool, Jurgen
Klopp amesema nyota wake huyo hauzwi kwa bei yoyote, pamoja na kwamba Coutinho
mwenye umri wa miaka 25-aliwasilisha maombi ya kuhama wiki iliyopita.
Barcelona imefanikiwa
kumsaini Paulinho kwa Pauni 36.5 milioni Alhamisi, lakini haitanawa mikono kwa Coutinho,
inayemtaka acheze sambamba na Lionel Messi na Luis Suarez Hispania.
Kabla ya ofa hiyo, Liverpool
ilikataa ofa mbili kwa ajili ya mchezaji huyo wa zamani wa Inter Milan – zenye thamani
ya Pauni 72 milioni na Pauni 90 milioni- na kusisitiza itabakia Anfield katika
msimu huu wa dirisha la usajili wa majira ya joto.
Coutinho bado
hajaitumikia Liverpool msimu huu baada ya kuumia mgongo akiwa mazoezini. Pia,
ataukosa mchezo wa Jumamosi dhidi ya Crystal Palace.
Alipoulizwa kuhusu
uhamisho wa Coutinho baada ya mchezo wa Jumamosi iliyopita dhidi ya Watford
ulioisha kwa sare ya mabao 3-3 d, Klopp alikiri kwamba suala hilo kwa sasa
haliko mikononi mwake
“Ninaweza kusema
jambo moja labda ni muhimu zaidi,” alisema Klopp.
“Kama kocha wa klabu
ya soka, nina mabosi wangu. Na kama mabosi wataamua, kwa mfano, muuze mchezaji
au hatumuuzi, ninapaswa kukubali.
Coutinho hataki
kuichezea Liverpool tena baada ya kuwasilisha maombi ya kuhama kwa njia ya
barua pepe kabla ya msimu mpya wa Ligi Kuu.
Post a Comment