0
LONDON, ENGLAND
ANTONIO CONTE ana kazi kubwa. Bilionea na mmiliki wa timu hiyo, Roman Abramovich aliitisha kikao cha benchi la ufundi alipofungwa na Liverpool.
Hali inaweza kuwa mbaya zaidi baada ya kufungwa mabao 3-0 na Arsenal.
Kocha Antonio Conte ameanza kujipanga upya ili kunusuru kibarua chake baada ya  kikosi kukumbana na kichapo, tena dhidi ya mahasimu wao wa jiji moja la London.
Kipigo hicho kimezua mjadala na huenda Abramovich akaitisha kikao na bodi nzima.
Katika kujinusuru, Kocha Conte sasa amefikiria kuwapiga chini mabeki wote waliocheza mechi hiyo ya Arsenal na kuruhusu mabao ya kijinga.

Conte akishangazwa na kipigo.
Mabeki Branislav Ivanovic na Gary Cahill walihusika kwenye bao la kwanza la Arsenal kwa kufanya uzembe, lakini beki yao iliendelea kufanya makosa ambayo yameifanya hadi sasa kuruhusu mabao 12 kwenye wavu wao.
Kitu ambacho Conte anachosubiri ni mabeki wake wengine wa kati John Terry na Kurt Zouma wapone na wakiwa fiti tu, moja kwa moja wanakuja kikosini na jambo hilo litawagharimu waliocheza kizembe kwenye kipigo cha Arsenal.

Cahill akijutia.
Kocha Conte anafikiria pia kumpiga chini beki wake mpya, Mbrazili, David Luiz kutoka kwenye orodha ya mabeki wake wa kati chaguo la kwanza na ikifika Januari tu shughuli ya kwanza itakayofanyika ni kuhakikisha anawanasa Leonardo Bonucci na Kalidou Koulibaly.
Beki mpya, Marcos Alonso ameonyesha kiwango kizuri kwa dakika chache alizocheza na huenda panga hilo lisipite kwenye jina lake.

Mabeki wa Chelsea wakijiuliza.
Ukiwaweka kando mabeki hao, Conte anawafikiria pia Michael Keane na Ben Gibson ambapo amewatuma skauti wake kuhakikisha wanawafuatilia kwa karibu wachezaji hao ili kuona kama wataweza kufiti kwenye kikosi chake ili kuondokana na shida ya kuruhusu mabao ya kijinga.
"Unauliza nilichukia kipindi cha kwanza? Jibu langu ni ndio, lakini huwa napenda kutozungumza sana, kwa sababu ninafahamu kitu ambacho napaswa kukizungumza, nitazungumza na wachezaji wangu kuwaeleza ukweli," alisema Conte.

Cahill
"Ni kawaida. Kweli nilikasirika, lakini wachezaji wangu walikasirika pia. Hii ni kwa sababu hatukufurahishwa na mchezo wetu na kiwango chetu. Sikulala, sikulala kabisa."
Kwenye orodha ya mabeki wa Chelsea waliopo kwenye kikosi hicho cha Mtaliano Conte ni Cesar Azpilicueta, Cahill, Ivanovic, Terry, Luiz, Zouma, Ola Aina na Marcos Alonso.

Cahill taabani.
Chelsea kwa sasa inashika nafasi ya nane kwenye msimamo wa Ligi Kuu England ikiwa na pointi 10, pointi nane pungufu ya kuwafikia vinara Manchester City, ambao wamekuwa na rekodi nzuri ya ushindi wa asilimia 100 tangu msimu huu uanze.
Nne Bora ya Ligi Kuu England kwa sasa inaundwa na Man City, Tottenham Hotspur, Arsenal na Liverpool, wakati vijana wa Jose Mourinho, Manchester United wakishika nafasi ya sita, huku Everton ya Ronald Koeman ipo ikiwa nafasi ya tano.


Post a Comment

 
Top