MUNICH, UJERUMANI
PEP Guardiola amekiri kwamba
amekataa kuongeza mkataba na Bayern Munich kwa sabababu anataka kufundisha Ligi
Kuu England.
Bosi huyo wa zamani wa Barcelona
ataachana na mabingwa hao wa Ujerumani
mwishoni mwa msimu huu na kujiunga na Manchester City.
Hata hivyo, Guardiola amesisitiza hajafanya
uchaguzi wa klabu gani atakwenda kufundisha England.
Akizungumza katika mkutano na
waandishi wa habari,alisema: “ sababu ya kutoongeza mkataba wangu ni nyepesi.
Ninataka kufundisha timu ya Primia Ligi.
“Nataka kupata uzoefu wa na kujua
hali ya hewa ikoje na kuangalia mbele.
Nina miaka 44, ni wakati mwafaka wa
kwenda kule.
“Kama ningekuwa na miaka 60 au 65 ningekaa
tu, lakini nadgni bado kijana zaidi.
“Siaamua ni klabui ipi ninayokwenda
kufundisha lakini ninahitaji changamoto mpaya.”
Kocha Carlo Ancelotti ametajwa
kurithi kibarua chake Bayern Munich na ataanza kazi mwishoni mwa msimu na
kuziacha klabu za England katika hali ya
taadhali.
Kocha wa Manchester City, Manuel
Pellegrini anatafutiwa mbadala, wakati Chelsea na Manchester United pia
zinatajwa kuangalia makocha wapya.
Lakini kama timu yoyote ya England itafanikiwa kumnsa Guardiola, kwa
maoni yake aliyoyatoa Jumanne katika
mkutano Jumanne yanaonyesha hatakaa kwa
muda mrefu na alisema hatamchukua
mchezaji yeyote kutoka Bayern.
“ Nataka uwanja mpya na kufahamu
miji na hoteli,” alisema.
“Miaka mitatu inatosha kwenye timu. Siyo
kocha wa kukaa katika klabu kwa miaka 30.”
Guardiola atawaongoza wachezaji wake
wa Bayern Munich kwenda kambini, Doha Jumatano kujiandaa na mchezo wa
Bundesliga dhidi Hamburg Januari 22.
Pamoja na kwamba kuondoka kwake
kunafahamika, Mhispania huyo yuko makini na kazi yake Allianz Arena kwa
kuzungumzia tamaa yake ya kushinda michezo ya Ulaya kabla ya kuondoka.
“Kwa hakika ninahitaji kushinda Ligi
ya Mabingwa msimu huu nikiwa na Bayern. Lakini siyo kazi rahisi.
Guardiola alisema amekuwa na furaha na maisha mazuri Bayern kutoana na uaminifu waliomuonyesha.
" Nadhani Rummenigge hatachukia. Wamefanya kila njia kunibakisha. Siyo sualala fedha ni uamuzi wangu."
Hata hivyo inafahamika kwamba Guardiola anakwenda katika timu ambayo inayofahamika ya Ligi Kuu England lakini amekuwa akificha.
" Nitakapota klabu ndipo klabu hiyo itaweka wazi," aliongeza. Nina ofa tofauti kutoka England lakini bado sijasaini.
Tangu atue Munich, Guardiola ameshinda mfululizo Kombe la Bundesliga na anaweza kuchukua kwa mara ya tatu msimu huu.
Pia, ameiongoza mara mbili Barcelona katika Ligi ya Mabingwa, ameshindwa kutwaa mara ya tatu taji hilo akiwa na Bayern.
Msimu uliopita matarajio yake yalikatishwa na timu yake ya zamani,Barcelona baada ya kuondolewa katika nusu fainali.
Post a Comment