PARIS,
UFARANSA
DAN
ALVES amemfanyia kitu mbaya Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola baada ya
kukamilisha usajili wake Paris Saint Germain (PSG).
Tukio
hilo limetokea siku chache baada ya beki huyo wa zamani wa Juventus kuchana na
miamba hiyo ya Turin, mwezi uliopita.
Beki huyo wa kulia wa
kimataifa Brazil mwenye umri wa miaka 34- kwa kiasi kikubwa alikuwa akitarajiwa
kuungana tena na kocha wake wa zamani wa Barcelona, Guardiola kikosini
Manchester City.
Habari za kujiunga na PSG badala ya Man
City zimewashtua wadau wengi zilipoanza kuripotiwa mapema wiki hii.
Jumamosi iliyopita, Alves alikuwa
akifunga ndoa na mpenzi wake katika Fukwe za Ibiza kule Hispania na Manchester
City ilikuwa ina uhakika kuwa mara baada ya tukio hilo, angesaini mkataba
uliokuwa mezani ili atue Ligi Kuu England.
PSG imetoa ofa zaidi ya
Manchester City ya Pauni 230,000 kwa wiki kwa beki huyo wa
zamani wa Sevilla kwa mkataba wa miaka
miwili.
Dani Alves akikabidhiwa jezi
Inadaiwa pia kuna uwezekano mkubwa
kuwa mke wa Alves amependelea zaidi kuishi Paris, jiji linalojulikana kwa
matanuzi makubwa na limekuwa kichocheo kwa wanasoka wanaotakiwa na PSG.
....akikaribishwa PSG
Hilo linakuwa pigo kubwa kwa Guardiola
dhidi ya Alves ambaye alitwaa mataji 23 akiwa na Barcelona, matatu yakiwa ya
Ulaya na sita ya La Liga huku akiwa mmoja kati ya wachezaji wa mwanzoni
kununuliwa na Guardiola pale Nou Camp akitokea Sevilla mwaka 2008 na hivi
karibuni aliwahi kumwelezea Guardiola kama kocha mwenye akili nyingi.
... akiwa na skafu ya PSG
Kutokana na hatua hiyo ya Alves, City
sasa inalazimika kuhamishia mipango yake na nguvu zote kwa beki wa kulia wa
Tottenham, Kyle Walker, ambaye Spurs ipo tayari kuachana naye kama City itafika
dau la Pauni 50 milioni. Akizungumza baada ya kumwaga wino PSG, Alves alisema: "Kuna mradi wa kuvutia hapa Paris, nina marafiki hapa na mimi ni mtu ninayependa changamoto. Kama nimewaumiza Guardiola na Manchester City, ninawaomba msamaha. Lakini nimekuja hapa kutwaa ubingwa."
"Nilikuwa na presha ya kushinda Ligi ya Mabingwa kwa miaka mitatu, nimekuja kuleta uzoefu wangu hapa. Rais (wa PSG) ana ushawishi mkubwa, nataka kuandika historia, tunaweza kuandika pamoja. Kazi ambayo klabu imefanya kwa miaka kadhaa inatia moyo. Ni timu yenye nia."
Guardiola anasaka mabeki wanne wa
pembeni baada ya kuachana na Gael Clichy, Bacary Sagna na Pablo Zabaleta na
mpaka sasa bado hajafanikiwa kumshawishi beki yeyote kutua kikosini hapo.
Kocha huyo wa zamani wa Bayern pia
inadaiwa kuwa anamsaka beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, ambaye pia
atamgharimu pesa nyingi wakati huu Monaco ikidhamiria kupata zaidi ya Pauni 40
milioni kwa staa huyo wa kimataifa wa Ufaransa.
Mastaa wengine ambao sasa wanaweza
kuangaliwa na Guardiola ni pamoja na beki wa kulia wa PSG, Serge Aurier, ambaye
nafasi yake itakuwa shakani baada ya kuwasili kwa Alves huku kukiwa na
malalamiko mengi ya kinidhamu kwa staa huyo wa Ivory Coast.
...PSG kuna ushawishi mkubwa hapa
Wengine ni pamoja na beki wa kulia wa
Benfica, Nelson Semedo, aliyekuwa anaelekea Barcelona lakini mpaka sasa dili
lake linasemekana halijakamilika. Vilevile kuna beki wa kulia wa Bayer
Leverkusen, Benjamin Henrichs na beki wa kulia wa Arsenal, Hector Bellerin.
Guardiola pia anajiandaa kupambana na
pigo jingine baada ya Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger, kutangaza wazi kwamba
hadhamirii kuachana na staa wake, Alexis Sanchez ambaye inadaiwa kuwa
Manchester City imekuwa ikimnyemelea kwa nguvu zote katika dirisha hili huku
akiwa amebakiza mkataba wa mwaka mmoja tu Emirates.Inadaiwa Alves atapata mara mbili PSG zaidi
ya kile ambacho Man City ilichopanga kumpatia.
...Alves amemuomba radhi Guardiola
Hata hivyo, uamuzi
wake labda umechangiwa na uwezekano mkubwa wa kushinda medali akiwa na PSG.
Dan Alves ambaye
ameshinda mataji akiwa na Barcelona na Juventus, sasa anaangalia uwezekano wa
kuongeza medali nyingine kwa kutwaa taji la Ufaransa wakati PSG ikipambana
kurudisha taji la Ligue 1 kutoka kwa Monaco.
Post a Comment